Wednesday, January 31, 2018

MAISHA NA NENO LA MUNGU

MAISHA NA NENO LA MUNGU

Kanisa Bwana Yesu asifiwe

  Niseme kidogo Juu ya Huduma ya Kundi
Kundi hili La  kiroho Na Sio La kidini  Kazi Kuu Ni kuhakikisha Watu wanapata injili Na kubadilika Kwa Neno wanalolipata

Katika injili Kuna Huduma Kama Za kuwasaidia Yatima Na wajane Kama inavyosemeka Katika Yakobo 1:27

Agizo Kuu La YESU Kwa Kila anayempokea Ni kuhakikisha anamfikishia mwingine taarifa/Habari njema njema ili apate tumaini La kudumu

Marko 16:15-16

Mathayo 28:19-20

Pia zimezungumza Juu ya Jukumu hilo

Hivyo Basi Kundi linashughulika Na jambo La kupeleka injili Kwa Watu ili kuwatangazia Habari njema

Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!
Warumi 10:15

Kama Huu Mstari unavyosema Ndio sababu Ukiwa mmoja wa Watu ambao Tayari unayo nuru unaombwa Kutoa mchango wako ili injili ifike sehemu moja Na nyingine

Ni Utaratibu wa Kundi Kwa Kila mwakundi Kutoa sh.  17,000/= ikiwa Ni kiwango cha chini Na Pia unaweza Kutoa zaidi ya hapo

Endapo Kila mmoja Wetu Hapa atatoa kiasi hicho Basi tunaweza kufanya Mkutano mkubwa Sana

Unahimizwa Kutoa Maadamu Ni makubaliano ya Watu wa  Mahali hapa

Kiongozi wetu mkuu hakuona vyema Kundi liwe cha kuchati Tu Bali Watu wapone Kupitia Huduma Za humu ndani.

Zipo shuhuda nyingi ambazo Watu wamepona, wamebadilika

*Wahudumu wa Mkutano*

Watu wanaohudumu Ni wenyeji Yaani wale wa  Kanisa tutakaloshirikiana nalo pamoja wa Watu wa Mahali Hapa Hapa
[

Kwa sababu Hatuna Kanisa Kama Mahali Pa kukutania hivyo inatubidi tutafute Kanisa La kushirikiana nalo ili Watu watakaookoka wasibaki kutangatanga

Hivyo mtu wa Pwani Hakikisha ushirika wako unaonekana ili tuweze Kuvuna Mavuno Katika shamba La MUNGU

Wahubiri tunapenda Sana watoke Mahali Hapa Kwa sababu Mkutano tunauandaa Sisi hivyo Ni vyema ikiwa  tutasimama Pia Katika kuhudumu madhabahuni

Waimbaji Nafasi Ni zenu Hakikisha unajipanga ili kuhudumu Katika kile Ambacho Mungu amekiweka ndani yako
Tunao Wachungaji, Wainjilisti,  Manabii, n.k

Hivyo MUNGU Akupe Kibali ili Utumike.

Hatufanyi Mkutano Kwa Kutaka faida hivyo usiwazie sadaka zitakazotolewa Kwenye Mkutano

Vipo vitu vingi ambavyo vitafanywa Kupitia sadaka

Mwaka Huu utakuwa Ni Mkutano WA tatu

Mara ya kwanza Ulifanyika

Mkoani TABORA  Mwaka 2017

      June

Mara ya pili Dar es salaam ,June  2017

    Mara ya tatu  Ni Pwani 2018

Kuna mtu ameelewa Baadhi ya mambo kuhusu Mkutano Na Kundi
Sasa Basi Mungu akujalie Kutoa ili kuuwezesha Mkutano Na ukumbuke Kuwa Hatuna wafadhili WA Aina yeyote Ile ila Ni Mimi na Wewe  tuliopo  Mahali Hapa

Maombi yanahitajika Sana tena Sana ili Mungu atende Makuu Kupitia Huu mkutano

Mwaka Jana Mkutano ulifanikiwa Ni Baada  ya watakatifu WA Bwana kusimama Katika zamu Zao Na Kumsihi Mungu

Nina mambo Matatu ya kumalizia kwako wewe

1. Maombi Kwa ajili ya Mkutano Na Mungu aandae Watu Lakini Pia aende Nasi

2. Kujitoa kwako ili kufanikisha hili tulilolikusudia. Wewe ambaye YESU amesha kupa nuru yake jitahidi ufanye kitu Kwa ajili ya Bwana wa Majeshi

3. Mchango wako WA Pesa ili watakaofanikiwa kupata Kibali waende Na kufanya Huduma Hiyo Kama Mungu alivyokusudia

Wewe mwenye Huduma Na upo Mbali Na Eneo Husika wasiliana Na uongozi Mapema Sana ili Kama lipo La kuwezekana lifanyiwe kazi

Bila Pesa hatutafanya Mkutano Na Pesa zipo kwako hivyo utoe

Naomba Niishie Hapa
Kama una Swali Karibu

Bwana awalinde Siku Hii aonekane kwako wewe uliye dhaifu, akugange Wewe uliyevujika Moyo,  akuondoe Kwenye mateso yote, akupe amani Na furaha

   IMEANDALIWA NA
MWL ERICK MACHUMU

MAFIA - PWANI

KATIBU MKUU..
+255 752 763 020

©2018

MAISHA NA NENO LA MUNGU

Published by

ZAWADI NGAILO

SIKONGE TABORA

ADMIN MKUU
+255 762 450 772
©2018
MAISHA NA NENO LA MUNGU

What's up

https://chat.whatsapp.com/2yJswYBSEzLL8e7GaM6gq1

    

No comments:

Post a Comment