Tuesday, February 6, 2018

Mombi

Maombi ni mawasiliano na Mungu

Ni mawasiliano na Muumba wetu ..

Mungu ni Roho

Yeremia 29:13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
    Tunapomtafuta Mungu kwa Moyo wetu tunamuona

Biblia imejaa maongezi mengi /mazungumzo mengi kati ya Mungu na Watu wake tangu Bustani ya Eden.
Mwanzo 2: 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.

Mungu amemuumba Mwanadamu kwa ajili ya Ushirika pamoja na Mazungumzo yake.

Wakati Mungu anaongea na Adamu na  Eva ilikuwa ni majibizano ya wazi.
Alizungumza nao na kuwapa maelekezo kwa njia ya Kawaida

Lakini kwa nyakati hizi njia ya kuwasiliana sisi na Mungu ni kupitia maombi

Maombi ni daraja LA kutuunganisha sisi pamoja naye

Zaburi 37 :4 Nawe utajifurahisha kwa BWANA,Naye atakupa haja za moyo wako.

23 Hatua za mtu zaimarishwa na BWANA,Naye aipenda njia yake.

Maombi ni njia ya kutufanya sisi tufurahie uwepo wa Mungu katika MAISHA yetu

Ni njia ya kumfanya Bwana ajibu haja za mioyo yetu ..

Mioyo yetu imebeba mahitaji mengi hatuwezi kuyatua pasipo kutumia maombi

    Maombi yanafanya hatua zetu ziimarishwe na Bwana .

Mungu mwenyewe ametualika sisi tumuite yeye na ameahidi kujibu au kutupa majibu ya kila tunachomuomba

Yeremia 3:3 Kwa sababu hiyo manyunyu yamezuiliwa, wala hapakuwa na mvua ya vuli; hata hivyo ulikuwa na kipaji cha uso cha kahaba, ulikataa kutahayarika.

Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

Waefeso 6:18

Zaburi 50:15

1 Yohana 5:14

✍Unapomuita Mungu jua anaitika

Na unapokwenda kumuomba

Naye atakusikiliza

Yesu Kristo alitufundisha namna ya kuomba kupitia Sala yake kuu

Luka 11:2 Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]
3 Utupe siku kwa siku riziki yetu.
4 Utusamehe dhambi zetu, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu].

Unapoomba Omba kwa Baba aliye Mbinguni

Jina lake litukuzwe

Ufalme wake uje nawe uishi humo

Mapenzi ya Mungu yatimizwe kwanza Kuliko yako

Pia akusamehe maovu na kukuepusha usiingie majaribuni

Pia rejea YOHANA Mtakatifu

Mlango wa  17 Hii inaonyesha Maombi ya karibu sana kati ya Mungu na Mwanae ( Yesu Kristo)

Ikiwa tumekuja kuwa wana wa Mungu kwa njia ya Imani katika Kristo tunaweza kuomba maombi ya karibu sana  na kumjua Mungu wetu naye atatisikia .

YOHANA 1:12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

Tunapokuwa karibu naye maana yake tunakuwa na Uwezo wa kufanya jambo lolote lile.

Miongoni mwa mifano itakayoonyesha jinsi Mungu anavyosema nasi na alivyoema na watu wengine .

✍Musa
Kutoka 4:10 Musa akamwambia BWANA Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.

✍Eliya Yakobo 5:17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

✍Daudi

   2Samweli 24:10 Ndipo moyo wake Daudi ukamchoma baada ya kuwahesabu hao watu. Naye Daudi akamwambia BWANA, Nimekosa sana kwa haya niliyoyafanya; lakini sasa, Ee BWANA, nakusihi uuondolee mbali uovu wa mtumishi wako; kwani nimefanya upumbavu kabisa.

✍Yesu
Mathayo 11:24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe.

Yohana 17:1

Viongozi wakubwa watu wakubwa waliamini kuwa maombi ni njia ya kuwafikisha mahali pa juu zaidi.

Wana sayansi wakubwa pamoja na Ujuzi waliokuwa nao lakini

Waliamini nguvu ya Maombi

Mfano wao

Abraham Lincoln

Isaac Newton

Louis Pasteur

Francis Bacon

George Washington

Carver ,Galileo

HAWA pia waliamini katika Maombi na Sala .

Kila anayetembea karibu na Mungu wanaisikia sauti yake ,

Sauti ya Mungu ni ya Upole na inasema ndani ya Roho za Watu waliojitoa kweli kweli kwa Bwana .



Matendo 8:29 Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.

Matendo 10:19 Na Petro alikuwa akiyafikiri yale maono. Roho akamwambia, Wako watu watatu wanakutafuta.

2 Wakorintho 12:9

Anasema na watu wake kupitia Roho Mtakatifu

      Anaishi ndani ya Roho na Mioyo ya watu waliokubali kujitoa kwake .

    Anawaongoza

Anawalinda na

Kuwahamasisha katika kutenda yapendezayo machoni pake.

Warumi 8:14 Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.

Wagalatia 5:18

Tunapoweka imani yetu  kwa Yesu Kristo kwa ajili ya Ukombozi ...
Roho Mtakatifu anakuja kwetu na kuishi ndani yetu .

Anatusaidia sisi kuwasiliana na  Mungu wetu  kwa kuyatimiza mapenzi yake .


Mungu akubariki kwa ujumbe huu

By Zawadi Ngailo
   Sikonge TABORA

  What's up
+255 762 450 772

No comments:

Post a Comment