Tuesday, March 13, 2018

ROHO MTAKATIFU

Roho Mtakatifu, kama Mshauri

Roho Mtakatifu, kama
Mshauri
Roho Mtakatifu ndiye ambaye
hufariji, anashauri na
Anaimarisha Wakristo, kuwaweka
wao karibu na Yesu Kristo.

Roho Mtakatifu ni Mshauri
pamoja na Yesu Kristo
Yesu Kristo ni Mshauri 1Jn
2: 1 Neno moja la Kigiriki "Parakletos"
inasisitiza maneno haya ambayo ni
kimsingi muda wa kisheria. Inaweza pia
kubeba maana ya "mfariji".

Roho ni Mshauri mwingine
Jn 14: 16-17 Neno "mwingine"
ina maana "nyingine ya sawa
aina ". Baada ya kupaa, a
Roho ni kudhani huduma
ya Yesu Kristo.

Mshauri ni zawadi ya
Yesu aliyeinuliwa Jn 16: 7 Angalia pia
Yohana 7: 38-39; Matendo  2:33

Mshauri hufariji na
huwahakikishia waumini

Jn 14: 16-18; Matendo 11:12 Petro ni
alihakikishiwa juu ya kwenda
nyumba ya Kornelio; Rum 8:16

Waumini wanahakikishiwa kuwa wao
ni watoto wa Mungu.

Mshauri huimarisha
na kuimarisha kanisa
Waefeso 3:16 Angalia Pia Matendo
4:31 .

Kanisa la Yerusalemu ni
imara katika uso wa
upinzani; Matendo 9:31 kanisa ndani
Yudea, Galilaya na Samaria; Rumi8:26

Mshauri anafundisha na
anawafundisha waumini
Roho huwakumbusha wanafunzi
mafundisho ya Yesu Kristo Jn
14:26

Angalia pia Yohana 16:14; 1Jn
5: 6-8
Roho hufundisha kanisa
ukweli zaidi

Jn 16:13 Ona pia
1Kor 2: 9-10; 1Jn 2:27

Mshauri husaidia
kanisa katika utume wake
Roho huhubiri kwa Yesu
Kristo na husaidia kanisa
fanya vivyo hivyo Jn 15: 26-27 Angalia
pia Matendo

1: 8
Roho huwahukumu
ulimwengu usioamini Jn 16: 8-11;
1Kor 14: 24-25
Mifano ya msaada wa Roho katika
shahidi na utume 

Petro mbele ya Sanhedrin; 1Co
2: 3-4 Paulo huko Korintho; 1Th 1: 5
Paulo na Sila huko Thesalonike

Mshauri huleta waumini
karibu na Yesu Kristo Ef
3: 16-17 Ona pia Yohana 14:23; Ro
8: 9-11

Monday, February 12, 2018

UAMINIFU

U aminifu ni mojawapo
ya tunda la Roho
katika maandiko
matakatifu.
Tutajifunza uaminifu wa
Mungu unaopatikana katika
neno lake. Yeye amesema
atatimiza yale aliyoahidi katika
neno lake, si tu kwa wana wa
Israel bali kwa watu  wote
wanaoishi sawasawa na neno
lake. Kwa hiyo, kwa upande
wetu inatupasa sisi nasi kuwa
waaminifu kwa kuliishi na
kulitenda neno la
Mungu. “Basi jueni ya kuwa
Bwana, Mungu wenu, ndiye
Mungu; Mungu mwaminifu,
ashikaye agano lake na
rehema zake kwao
wampendao, na kushika
amri zake, hata vizazi
elfu. Na itakuwa, kwa sababu
mwazisikiza hukumu hizi, na
kuzishika na kuzitenda, basi
Bwana, Mungu wako,
atakutimizia agano na
rehema aliyowaapia baba
zako.” Kum 7:9, 12. “Ndivyo
litakavyokuwa neno langu,
litokalo katika kinywa
changu  halitanirudia bure
bali litatimiza mapenzi
yangu, nalo litafanikiwa
katika mambo yale
niliyolituma.” Isa 55:11.
Tabia ya mtu mwaminifu.
1. Mtu aliye mwaminifu ni yule
ambaye anatenda sawasawa na
maagizo, sheria na taratibu .
Ikiwa ni mtu aliyeajiriwa
katika kazi za nyumbani au ya
serikali anafanya kazi
ipasavyo, si mwizi, mpokea
rushwa, mdhulumaji na wala
si mwenye hila. Unaweza
kuona ilivyoandikwa kuhusu
mtumishi aliyeajiriwa kazi za
nyumbani ambaye alipaswa
kufanya kwa uaminifu. “Ni
nani basi yule mtumwa
mwaminifu mwenye akili,
ambaye bwana wake
alimweka juu ya nyumba
yake, awape watu chakula
kwa wakati wake? Heri
mtumwa yule, ambaye bwana
wake ajapo atamkuta
akifanya hivyo.” Mt 24:45-46.
2. Hatendi dhambi.Yusufu
mtumishi wa Potifa kwa kuwa
alikuwa mwaminifu
aliposhawishiwa na mke wa
Potifa ili kufanya naye dhambi
ya uzinzi alikataa. “....mke wa
bwana wake akamtamani
Yusufu, akamwambia, lala
nami. Lakini alikataa
akamwambia....Nifanyeje
ubaya huu mkubwa
nikamkose Mungu?” Mwa
39:7-9.
3.  Hachukui kitu cha mtu
mwingine, iwe ni fedha, mali,
au kitu kingine chochote
ambacho   si halali yake. Akitoa
fedha kwa ajili ya malipo
yoyote na akarudishiwa pesa
ya ziada  hurudisha  kiasi
kilichozidi.  Ikiwa  amemwona
mtu  ambaye amedondosha
fedha  au amepoteza kitu
chochote humrudishia. Kwa
kufanya hivyo analitii na
kulitenda neno la Mung
linavyosema, “Umwonapo
ng’ombe wa nduguyo au
kondoo wake
akipotea....sharti umrudishe
kwa nduguyo. Na kwamba
yule nduguyo hayuko karibu
nawe, na ukiwa humjui,
umchukue kwenu nyumbani
kwako, uwe naye hata aje
nduguyo kumtafuta, nawe
mrudishie....tena fanya vivyo
kwa kila kitu kilichopotea
cha nduguyo,....” Kum 22:1-3.
Umuhimu wa kuwa
mwaminifu.
Mkristo ambaye ameokoka
akiwa ni mwaminifu,  Mungu
anamwamini na kumweka
katika kazi ya
utumishi.  Tunaweza kujifunza
kwa baadhi ya watu ambao
Mungu aliwaona ni waaminifu
na kuwachagua na kuwafanya
kuwa watumishi wa kazi yake,
mfano  wa Yesu, Musa
na  Paulo “....Yesu aliyekuwa
mwaminifu kwake yeye
aliyemweka, kama Musa
naye alivyokuwa, katika
nyumba yote ya Mungu. Na
Musa kweli alikuwa
mwaminifu katika nyumba
yote ya Mungu
kama  mtumishi....” Ebr
3:1,5. Mtume Paulo alikuwa ni
mwaminifu ndio
maana  ameandika
akisema, “Namshukuru Kristo
Bwana wetu, aliyenitia nguvu
kwa sababu aliniona kuwa
mwaminifu, akaniweka
katika utumishi wake.” 1Tim
1:12.
Yampasayo mtu ili aweze
kudumu katika uaminifu.
Bwana wetu Yesu Kristo
alipokuwa hapa duniani kwa
sababu alikuwa ni mwaminifu
kila alipojaribiwa na
alizitambua hila za shetani
wala hakufanya kosa lolote.
Ndio maana ulipokaribia
wakati wa kukamatwa
aliwaambia wanafunzi wake
akisema, “....yuaja mkuu wa
ulimwengu huu hana kitu
kwangu.” Yn 14:30.
Kwa mkristo ambaye
ameokoka, amejazwa Roho
mtakatifu na kudumu katika
uaminifu, Roho mtakatifu
humfunulia hila zote za
Shetani anapojaribiwa.
Waliosimama imara katika
neno la Mungu Shetani huja na
kuwajaribu katika shida na
dhiki. Usikubali mawazo ya
shetani, bali mpinge na
kumkemea, kwa kumwambia,
nenda zako Shetani. “Ndipo
Yesu alipomwambia, Nenda
zako, Shetani,....Kisha Ibilisi
akamwacha....” Mt
4:10-11. “Basi mtiini Mungu.
Mpingeni Shetani, naye
atawakimbia,  Mkaribieni
Mungu naye atawakaribia
ninyi....” Yak 4:7-8. Kutokana
na andiko hili mtu anaweza
kuwa karibu na Mungu  na
kumkemea Shetani naye
huondoka, ikiwa analitii neno
na kuishi linavyosema.
Wale wote waliozaliwa mara
ya pili imewapasa kuushinda
ulimwengu na dhiki kwa
sababu aliye ndani yao ni
mkuu kuliko shetani, naye
Yesu alimshinda na
kushuhudia
akisema , “Ulimwenguni
mnayo dhiki; lakini jipeni
moyo; mimi nimeushinda
ulimwengu.” Yn 16:33 . Kwa
upande mwingine,
tunapolifahamu neno la Mungu
tunazitambua hila za shetani
na kumshinda. “Nao
wakamshinda kwa damu ya
mwana-kondoo, na kwa neno
la ushuhuda wao, ambao
hawakupenda maisha yao
hata kufa.” Ufu
12:11. “....Uwe mwaminifu
hata kufa, nami nitakupa taji
ya uzima....Yeye ashindaye
hatapatikana na madhara ya
mauti ya pili (Jehanum) .” Ufu
2:11-11.
Kinachotokea kwa  mtu
anayedumu katika uaminifu.
1. Mungu humbariki na uzao
wake . “Mtu mwaminifu
atakuwa na Baraka tele” Mit
28:20.
“Mwenye haki aendaye
katika
unyofu (uaminifu) wake,
Watoto wake wabarikiwa
baada yake.” Mit 20:7.
2. Mungu anakuwa karibu
naye wakati anapomwita au
kumwomba. “Bwana yu
karibu na wote wamwitao,
Wote wamwitao kwa
uaminifu.” Zab 145:18.
3. Anampendeza
Mungu. “Walio wakamilifu
katika njia zao
humpendeza.” Mit 11:20.

Sunday, February 11, 2018

SOMO :IMANI

MAANA YA  IMANI

IMANI ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, Ni bayana ya mambo yasiyoonekana
Hiyo ni kwa mujibu wa Waebrania11:1

Katika maana hiyo ya imani tunazo sentensi mbili

Na ndani yake kuna maneno yanayobeba maana ya neno *imani*

Uhakika= ni ushahidi wa kutosha juu ya jambo tukio /fulani

Bayana= ni uwazi , dhahiri.Kwahiyo tunaposema hakika/uhakika maaa yake ni ushahidi wa kutosha

Mtu anapojaribu kuelezea tukio fulani watu huuliza, "una uhakika?"

Au wengine husema tutakuaminije?

Kwa maneno mengine Imani ni jicho la kuona vitu visivyoonekana
2wakorintho 5:7 (Maana twaenenda kwa imani, si kwa kuona.)

Efeso 1:18 macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo;

Ndiyo maana katika warumi anasema

Kwa sababu ukimkiri Yesu kwa kinywa chako na kuamini *moyoni* mwako..

Hapo utaona kuwa imani inakaa moyoni

Mwili wa mtu huwa gizani ikiwa macho yake ya moyo hayajatiwa nuru, na nuru hiyo ni
*Imani kwa kadiri imani ya mtu inavyoongezeka ndivyo anavyozidi kuona yuko katika nuru.

Ni kama vile nuru ya jua inavyoweza kufifia na kung'aa kwa nyakati tofauti tofauti
[2/11, 20:01] Masalu: *CHANZO*  CHA *IMANI*

Warumi 10:17

Imani chanzo chake ni kusikia,

Na kusikia huja kwa neno la kristo

Kwa kadri mtu anavyozidi kusikia ndivyo imani yake huongezeka pia

Mtu akifuliza kusikia habari za uganga na uchawi imani yake hukuwa zaidi katika mambo hayo.

Ndiyo maana unakuta mtu anayeziamini habari za uganga si rahisi kumhamisha huko

Lakini imani yetu sisi hutokana na neno la kristo

Kwa kadri mtu anavyokuwa na bidii kusikia neno ndivyo imani yake pia hukua

Kwahiyo

Kiwango cha imani hutegemea kiwango cha Neno lililo ndani ya mtu.

Biblia inapozungumzia kusikia ni tofauti na kusikiliza au kujifunza peke yake, isipokuwa kulitunza Neno na kulitenda
Soma kumbukumbu 28: 1 Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

Kwa hiyo waweza jipima kwamba kiasi cha imani uliyo nayo ndiyo kiwango cha neno ulililo nalo.

Neno ni pumzi ya Mungu, hivyo kiwango cha imani yako ni kiwa cha Mungu ndani yako

*NGUZO* ZA *IMANI*

(MISINGI YA IMANI, MAWAKILI WA IMANI)

👆👆
Hivi ni vtu ambavyo vinasaidia  utendaji kazi wa imani

Kama vile nyumba ili iwe imara inahitaji msingi lakini vilevile nguzo

1⃣UPENDO WA KI-MUNGU
Au nguvu ya uungu

1Yohana 4:7-8

7 Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.

7  Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.

1 Yohana 4 :7

8  Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.

1 Yohana 4 :8

Mungu ni upendo
Hivyo basi ili mtu awe na Mungu ndani yake ni lazima awe na upendo

Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.

Wagalatia 5 :6

Biblia inatuagiza katika wakorintho kwamba:

Kesheni simameni imara katika imani,...

Mambo yenu yote yatendeke katika upendo.

1 Wakorintho 16:13  Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari.

14  Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.

👆👆
Hapo tunaona jinsi ambavyo neno imani linaambatana na upendo

Maana yake imani haiwezi kusimama peke yake pasipo upendo.

Katika hali ya kawaida ukipenda jambo fulani lazima una imani juu ya jambo hilo

Ukimpenda mtu vilevile utakuwa unamwamini
Lakini upendo ukiondoka huna imani naye tena hilo liko wazi

Hivyo msingi imara wa imani ni *UPENDO* tena wa ki-Mungu
Imani pasipo upendo haitendi kazi
1wakorintho 13: 2  Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

Paulo anasema,

Hata angekuwa na imani kiasi gani lakini pasipo upendo ni sifuri au F

2⃣MATENDO

Hii ni nguzo nyingine ya imani
Yakobo 2:14, 22, 26

Kama vile mwili pasipo roho umekufa, kadhalika imani pasipo matendo nayo imekufa

Mtu anaposema ana imani lazima hiyo imani aiweke katika matendo lasivyo itakuwa ni imani mfu.

Tunahitaji kuona kile unachokiamini  kinafanya kazi katika maisha yako

Hapo utaona yanatajwa mambo matatu,

Imani

Tumaini

Upendo

Lakini katika hayo yote lililo kuu ni upendo

*MAADUI* WA *IMANI*

1. HOFU NA MASHAKA
Mathayo 14:26-32

Mtu mmoja aniwekee mistari hiyo

Yakobo 1:5-6
  1 Wakorintho 13:13  Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.

Mathayo 14:26  Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu.
27  Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope.
Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.

28 Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu.

29 Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.

30 Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?

31 Nao walipopanda chomboni, upepo ulikoma.
32 Kilicho mfanya Petro aanze kuzama ni hofu
Maana aliamini kuwa ni Yesu ndiyo na akachukua hatua lakini imani yake ilishambuliwa na hofu

Yakobo 1:5  Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa

6  Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

Yesu akamshika mkono akamwambia

Ewe mwenye imani haba mbona uliona shaka?

Hapo utaona neno hofu na mashaka yalivyotumika kwa pamoja
Ndivyo ilivyo hata sasa kwamba mtu anaamini lakini dhoruba ikipiga imani inayumba kwa sababu ya kuruhusu hofu moyoni ambako ndiko imani inakaa

Mtu anapoomba

Na aombe kwa imani pasipo shaka yoyote

Kwahiyo palipo na shaka hapana imani, na kama imani ikiwepo kisha hofu akabisha hodi na kuingia basi imani huanza kuondoka taratibu

Waebrania 10:38

Yakobo1:5-6
5lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima,na aombe dua kwa Mungu,awapaye wrote,kwa ukarimu,wala hakemei;naye atapewa
6ila na aombe kwa imani pasipo shaka yo yote ;maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari liliochukuliwa name upepo na kupeperushwa huku na huku

Jambo jingine ni *kusitasita*
Hili nalo ni adui wa imani

Tena hapa Mungu anasema mwenye haki akisitasita roho yake haina furaha naye.

Kwa maana hiyo huwa tunapomhuzunisha Mungu pale tunapokuwa tumemwamini halafu bado tukaendelea kusitasita kwa kuona kwamba itakuwaje
Lakini kumbe kwake hakuna lisilowezekana

Mungu hututazama na kutuona vile tunahangaika huku tunasema tumemwamini anabaki anasikitika

Hapo ndipo inategemea unamjua Mungu kwa kiwango gani

Nimalizie kwa kukupa
 

*KAZI* ZA *IMANI*

1. Kuuona utukufu wa Mungu
Yohana 11:39-40
Utukufu-upako ama nguvu za Mungu
2.  Kufuatwa na ishara
Marko 16:17-18
3.  Kumshinda shetan 1Petro 5:7-8

4.    Imani ni uhai wa mwili na roho.
Ebrania 10:38a

5.   Imani huponya
Marko 5:34, 10:52

Kwa muda wako pitia maandiko hayo ili upate kujifunza,

Mungu wa mbinguni awabariki

@Mwalimu Samweli Masalu

Dodoma-Tanzania

Tuesday, February 6, 2018

Mombi

Maombi ni mawasiliano na Mungu

Ni mawasiliano na Muumba wetu ..

Mungu ni Roho

Yeremia 29:13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
    Tunapomtafuta Mungu kwa Moyo wetu tunamuona

Biblia imejaa maongezi mengi /mazungumzo mengi kati ya Mungu na Watu wake tangu Bustani ya Eden.
Mwanzo 2: 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.

Mungu amemuumba Mwanadamu kwa ajili ya Ushirika pamoja na Mazungumzo yake.

Wakati Mungu anaongea na Adamu na  Eva ilikuwa ni majibizano ya wazi.
Alizungumza nao na kuwapa maelekezo kwa njia ya Kawaida

Lakini kwa nyakati hizi njia ya kuwasiliana sisi na Mungu ni kupitia maombi

Maombi ni daraja LA kutuunganisha sisi pamoja naye

Zaburi 37 :4 Nawe utajifurahisha kwa BWANA,Naye atakupa haja za moyo wako.

23 Hatua za mtu zaimarishwa na BWANA,Naye aipenda njia yake.

Maombi ni njia ya kutufanya sisi tufurahie uwepo wa Mungu katika MAISHA yetu

Ni njia ya kumfanya Bwana ajibu haja za mioyo yetu ..

Mioyo yetu imebeba mahitaji mengi hatuwezi kuyatua pasipo kutumia maombi

    Maombi yanafanya hatua zetu ziimarishwe na Bwana .

Mungu mwenyewe ametualika sisi tumuite yeye na ameahidi kujibu au kutupa majibu ya kila tunachomuomba

Yeremia 3:3 Kwa sababu hiyo manyunyu yamezuiliwa, wala hapakuwa na mvua ya vuli; hata hivyo ulikuwa na kipaji cha uso cha kahaba, ulikataa kutahayarika.

Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

Waefeso 6:18

Zaburi 50:15

1 Yohana 5:14

✍Unapomuita Mungu jua anaitika

Na unapokwenda kumuomba

Naye atakusikiliza

Yesu Kristo alitufundisha namna ya kuomba kupitia Sala yake kuu

Luka 11:2 Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]
3 Utupe siku kwa siku riziki yetu.
4 Utusamehe dhambi zetu, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu].

Unapoomba Omba kwa Baba aliye Mbinguni

Jina lake litukuzwe

Ufalme wake uje nawe uishi humo

Mapenzi ya Mungu yatimizwe kwanza Kuliko yako

Pia akusamehe maovu na kukuepusha usiingie majaribuni

Pia rejea YOHANA Mtakatifu

Mlango wa  17 Hii inaonyesha Maombi ya karibu sana kati ya Mungu na Mwanae ( Yesu Kristo)

Ikiwa tumekuja kuwa wana wa Mungu kwa njia ya Imani katika Kristo tunaweza kuomba maombi ya karibu sana  na kumjua Mungu wetu naye atatisikia .

YOHANA 1:12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

Tunapokuwa karibu naye maana yake tunakuwa na Uwezo wa kufanya jambo lolote lile.

Miongoni mwa mifano itakayoonyesha jinsi Mungu anavyosema nasi na alivyoema na watu wengine .

✍Musa
Kutoka 4:10 Musa akamwambia BWANA Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.

✍Eliya Yakobo 5:17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

✍Daudi

   2Samweli 24:10 Ndipo moyo wake Daudi ukamchoma baada ya kuwahesabu hao watu. Naye Daudi akamwambia BWANA, Nimekosa sana kwa haya niliyoyafanya; lakini sasa, Ee BWANA, nakusihi uuondolee mbali uovu wa mtumishi wako; kwani nimefanya upumbavu kabisa.

✍Yesu
Mathayo 11:24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe.

Yohana 17:1

Viongozi wakubwa watu wakubwa waliamini kuwa maombi ni njia ya kuwafikisha mahali pa juu zaidi.

Wana sayansi wakubwa pamoja na Ujuzi waliokuwa nao lakini

Waliamini nguvu ya Maombi

Mfano wao

Abraham Lincoln

Isaac Newton

Louis Pasteur

Francis Bacon

George Washington

Carver ,Galileo

HAWA pia waliamini katika Maombi na Sala .

Kila anayetembea karibu na Mungu wanaisikia sauti yake ,

Sauti ya Mungu ni ya Upole na inasema ndani ya Roho za Watu waliojitoa kweli kweli kwa Bwana .



Matendo 8:29 Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.

Matendo 10:19 Na Petro alikuwa akiyafikiri yale maono. Roho akamwambia, Wako watu watatu wanakutafuta.

2 Wakorintho 12:9

Anasema na watu wake kupitia Roho Mtakatifu

      Anaishi ndani ya Roho na Mioyo ya watu waliokubali kujitoa kwake .

    Anawaongoza

Anawalinda na

Kuwahamasisha katika kutenda yapendezayo machoni pake.

Warumi 8:14 Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.

Wagalatia 5:18

Tunapoweka imani yetu  kwa Yesu Kristo kwa ajili ya Ukombozi ...
Roho Mtakatifu anakuja kwetu na kuishi ndani yetu .

Anatusaidia sisi kuwasiliana na  Mungu wetu  kwa kuyatimiza mapenzi yake .


Mungu akubariki kwa ujumbe huu

By Zawadi Ngailo
   Sikonge TABORA

  What's up
+255 762 450 772

Wednesday, January 31, 2018

MAISHA NA NENO LA MUNGU

MAISHA NA NENO LA MUNGU

Kanisa Bwana Yesu asifiwe

  Niseme kidogo Juu ya Huduma ya Kundi
Kundi hili La  kiroho Na Sio La kidini  Kazi Kuu Ni kuhakikisha Watu wanapata injili Na kubadilika Kwa Neno wanalolipata

Katika injili Kuna Huduma Kama Za kuwasaidia Yatima Na wajane Kama inavyosemeka Katika Yakobo 1:27

Agizo Kuu La YESU Kwa Kila anayempokea Ni kuhakikisha anamfikishia mwingine taarifa/Habari njema njema ili apate tumaini La kudumu

Marko 16:15-16

Mathayo 28:19-20

Pia zimezungumza Juu ya Jukumu hilo

Hivyo Basi Kundi linashughulika Na jambo La kupeleka injili Kwa Watu ili kuwatangazia Habari njema

Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!
Warumi 10:15

Kama Huu Mstari unavyosema Ndio sababu Ukiwa mmoja wa Watu ambao Tayari unayo nuru unaombwa Kutoa mchango wako ili injili ifike sehemu moja Na nyingine

Ni Utaratibu wa Kundi Kwa Kila mwakundi Kutoa sh.  17,000/= ikiwa Ni kiwango cha chini Na Pia unaweza Kutoa zaidi ya hapo

Endapo Kila mmoja Wetu Hapa atatoa kiasi hicho Basi tunaweza kufanya Mkutano mkubwa Sana

Unahimizwa Kutoa Maadamu Ni makubaliano ya Watu wa  Mahali hapa

Kiongozi wetu mkuu hakuona vyema Kundi liwe cha kuchati Tu Bali Watu wapone Kupitia Huduma Za humu ndani.

Zipo shuhuda nyingi ambazo Watu wamepona, wamebadilika

*Wahudumu wa Mkutano*

Watu wanaohudumu Ni wenyeji Yaani wale wa  Kanisa tutakaloshirikiana nalo pamoja wa Watu wa Mahali Hapa Hapa
[

Kwa sababu Hatuna Kanisa Kama Mahali Pa kukutania hivyo inatubidi tutafute Kanisa La kushirikiana nalo ili Watu watakaookoka wasibaki kutangatanga

Hivyo mtu wa Pwani Hakikisha ushirika wako unaonekana ili tuweze Kuvuna Mavuno Katika shamba La MUNGU

Wahubiri tunapenda Sana watoke Mahali Hapa Kwa sababu Mkutano tunauandaa Sisi hivyo Ni vyema ikiwa  tutasimama Pia Katika kuhudumu madhabahuni

Waimbaji Nafasi Ni zenu Hakikisha unajipanga ili kuhudumu Katika kile Ambacho Mungu amekiweka ndani yako
Tunao Wachungaji, Wainjilisti,  Manabii, n.k

Hivyo MUNGU Akupe Kibali ili Utumike.

Hatufanyi Mkutano Kwa Kutaka faida hivyo usiwazie sadaka zitakazotolewa Kwenye Mkutano

Vipo vitu vingi ambavyo vitafanywa Kupitia sadaka

Mwaka Huu utakuwa Ni Mkutano WA tatu

Mara ya kwanza Ulifanyika

Mkoani TABORA  Mwaka 2017

      June

Mara ya pili Dar es salaam ,June  2017

    Mara ya tatu  Ni Pwani 2018

Kuna mtu ameelewa Baadhi ya mambo kuhusu Mkutano Na Kundi
Sasa Basi Mungu akujalie Kutoa ili kuuwezesha Mkutano Na ukumbuke Kuwa Hatuna wafadhili WA Aina yeyote Ile ila Ni Mimi na Wewe  tuliopo  Mahali Hapa

Maombi yanahitajika Sana tena Sana ili Mungu atende Makuu Kupitia Huu mkutano

Mwaka Jana Mkutano ulifanikiwa Ni Baada  ya watakatifu WA Bwana kusimama Katika zamu Zao Na Kumsihi Mungu

Nina mambo Matatu ya kumalizia kwako wewe

1. Maombi Kwa ajili ya Mkutano Na Mungu aandae Watu Lakini Pia aende Nasi

2. Kujitoa kwako ili kufanikisha hili tulilolikusudia. Wewe ambaye YESU amesha kupa nuru yake jitahidi ufanye kitu Kwa ajili ya Bwana wa Majeshi

3. Mchango wako WA Pesa ili watakaofanikiwa kupata Kibali waende Na kufanya Huduma Hiyo Kama Mungu alivyokusudia

Wewe mwenye Huduma Na upo Mbali Na Eneo Husika wasiliana Na uongozi Mapema Sana ili Kama lipo La kuwezekana lifanyiwe kazi

Bila Pesa hatutafanya Mkutano Na Pesa zipo kwako hivyo utoe

Naomba Niishie Hapa
Kama una Swali Karibu

Bwana awalinde Siku Hii aonekane kwako wewe uliye dhaifu, akugange Wewe uliyevujika Moyo,  akuondoe Kwenye mateso yote, akupe amani Na furaha

   IMEANDALIWA NA
MWL ERICK MACHUMU

MAFIA - PWANI

KATIBU MKUU..
+255 752 763 020

©2018

MAISHA NA NENO LA MUNGU

Published by

ZAWADI NGAILO

SIKONGE TABORA

ADMIN MKUU
+255 762 450 772
©2018
MAISHA NA NENO LA MUNGU

What's up

https://chat.whatsapp.com/2yJswYBSEzLL8e7GaM6gq1

    

Saturday, January 27, 2018

ITAKIENI AMANI YERUSALEMU


  Mungu anatwambia tuiombea Amani Yerusalemu

Zaburi 122: 6 Utakieni Yerusalemu amani;Na wafanikiwe wakupendao;
7 Amani na ikae ndani ya kuta zako,Na kufanikiwa ndani ya majumba yako.
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zanguNiseme sasa, Amani ikae nawe.
9 Kwa ajili ya nyumba ya BWANA, Mungu wetu,Nikutafutie mema.

     Katika NENO hili tunaona kwamba kuomba Amani na mema kuja kwenye mji Mtakatifu ni FAIDA kwa wanaouombea ..

Mungu ameahidi  Baraka kwa wote wanaoitakia Baraka Israeli na laana wanao ilani.

Mwanzo 12:3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.

      Yerusalemu ni mji wa Wayahudi ,unafuatiwa na wale wanaouombea Amani na Ulinzi
Na Amani.

    Yerusalemu ni MAKAO ya Mungu  ya Amani.

Zaburi 125:5 Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka,BWANA atawaondoa pamoja na watenda maovu.Amani ikae na Israeli

Yerusalemu ni mahali pa Kurudi kwa Yesu mara ya Pili

Zakaria 14:4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini.

Matendo 1:11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.

Na Wakati Huo ataaanzisha Amani ya kudumu .
  Yesu anasema sisi tuwe watengenezaji wa Amani .
   Amani inatengenezwa kwa Kuombea Amani

Mathayo 5: 9 Heri wapatanishi;Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

Pia tunatakiwa kuishi kwa Amani na watu wote .

   Warumi 12:18 Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.

Mungu anataka sisi kutafuta Amani na watu wote na tushiriki  katika maombi ya Amani  ndani ya Yerusalemu. Kwa kuwa ndio kiini cha moyo wake na MAKAO  yake.

Mungu akubariki

Wednesday, January 10, 2018

YESU NI MASIHI

   Yesu anaitwa Masihi Mathayo 1:16 Yakobo akamzaa Yusufu mumewe Mariamu aliyemzaa YESU aitwaye Kristo.
    Neno Kristo Lina maana ya Masihi .

Masihi ni Mpakwa mafuta

Agano la Kale lilitabiri habari za kuja kwa Masihi .

Na Agano jipya linatukumbusha kwamba Masihi ni Yesu Kristo .

Kuna mambo mengi ambayo wayahudi ( Watu wa uyahudi)
Walitarajia yatakuwa kwa Masihi kulingana na Ahadi iliyopo kwa Manabii wa Agano la Kale.

   Masihi atakuwa Mwebrania/Mwanaume wa Kiebrania

√ Isaya 9:6 Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,Tumepewa mtoto mwanamume;Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake;Naye ataitwa jina lake,Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu,Baba wa milele, Mfalme wa amani.

√Atazaliwa Bethlehem Mica 5:2 Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.

√Atazaliwa na Bikra  Isaya 7:14 Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.

Atakuwa nabii atakayetoka miongoni mwa ndugu
Kumbukumbu la Torati 18:18 Mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.

√Atakuwa kuhani mfano wa Melkizedeki ( Melchizedek )

Zaburi 110:4 BWANA ameapa,Wala hataghairi,Ndiwe kuhani hata milele,Kwa mfano wa Melkizedeki.

√Atakuwa Mfalme

Isaya 11:1Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.
2 Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA;
3 na furaha yake itakuwa katika kumcha BWANA; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake;
4 bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya.

*Mwana wa Daudi

Mathayo 22:42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.

•Aliyeteseka kabla ya kuingia katika Utukufu wake
Isaya 53:1 Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta?Na mkono wa BWANA amefunuliwa nani?
2 Maana alikua mbele zake kama mche mwororo,Na kama mzizi katika nchi kavu;Yeye hana umbo wala uzuri;Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.
3 Alidharauliwa na kukataliwa na watu;Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko;Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao,Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.
4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu,Amejitwika huzuni zetu;Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa,Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu,Alichubuliwa kwa maovu yetu;Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake,Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
6 Sisi sote kama kondoo tumepotea;Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe;Na BWANA ameweka juu yakeMaovu yetu sisi sote.
7 Alionewa, lakini alinyenyekea,Wala hakufunua kinywa chake;Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni,Na kama vile kondoo anyamazavyoMbele yao wakatao manyoya yake;Naam, hakufunua kinywa chake.
8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa;Na maisha yake ni nani atakayeisimulia?Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai;Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
9 Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya;Na pamoja na matajiri katika kufa kwake;Ingawa hakutenda jeuri,Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
10 Lakini BWANA aliridhika kumchubua;Amemhuzunisha;Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi,Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi,Na mapenzi ya BWANA yatafanikiwa mkononi mwake;
11 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika.Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye hakiAtawafanya wengi kuwa wenye haki;Naye atayachukua maovu yao.
12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu,Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari;Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa,Akahesabiwa pamoja na hao wakosao.Walakini alichukua dhambi za watu wengi,Na kuwaombea wakosaji.

     Yesu Kristo alitimiza mahitaji yote /vigezo vyote vya Umasihi

Kwa sababu alikuwa ni wa kabila la Yuda

Luka 3:30 wa Simeoni, wa Yuda, wa Yusufu, wa Yonamu, wa Eliakimu,

√Alizaliwa Bethlehem  Luka 2:4 Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa mbari na jamaa ya Daudi;
5 ili aandikwe pamoja na Mariamu mkewe, ambaye amemposa, naye ana mimba.
6 Ikawa, katika kukaa huko, siku zake za kuzaa zikatimia,
7 akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori ya kulia ng?ombe, kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.

√Alizaliwa na Bikra Luka 1: 26 Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu.

   Ushahidi mwingine wa kwamba Yesu ni masihi alikuwa nabii kama Musa( Moses)..

Musa na Yesu wote ni manabii

Kumbukumbu la Torati 34:10 Wala hajainuka tena katika Israeli nabii kama Musa, ambaye BWANA alimjua uso kwa uso;

Yesu Kristo ni nabii mkubwa kuliko Musa ...

Musa aliwatoa Israeli Utumwani lakini Yesu ametuokoa na kutuweka mbali hukumu ya Kifo na Dhambi .

Mbali na Musa Yesu Kristo hamwakilishi Mungu Bali ni Mungu  mwenyewe ..

Yohana Mtakatifu 10: 30 Mimi na Baba tu umoja.

Yesu Kristo hatuongozi tu kutufikisha Nchi ya Ahadi Bali anatuongoza sisi tufike Mbinguni na kuurithi Uzima wa Milele

√Yohana Mtakatifu  14:1 Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.

Yesu Kristo ni nabii mkubwa kuliko Musa

Kama masihi alikuwa kuhani wa Kifalme ..

Hakuwa mlawi na mlawi tu ndio aliruhusiwa kuwa kuhani.

Yesu Kristo ni kuhani mfano wa Melkizedek

Mwanzo 14

Zaburi 110:4

Ni Mfalme wa Amani Waebrania 7:2 ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;

Yesu Kristo ni mkubwa kuliko Abraham

Yohana 8:58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.