BWANA YESU ASIFIWE
Mpendwa Zipo shida nyingi sana katika Maisha yetu ambazo mlango wake wa kutokea ni YESU Kristo peke yake
Kitabu cha Ufunuo 3:20 kinasema hivi .."
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
YESU Kristo anasema tazama Nasimama mlangoni ,Nabisha ,MTU akisikia sauti Yangu na kuufungua mlango ,Nitaingia kwake nami nitakula pamoja naye ,Na yeye pamoja nami .
Mlango waweza kuwa ni moyo wako ,Mwili wako waweza kuwa mlango ,Familia ,Ukoo na ndugu zako vinaweza kuwa Mlango wa kuleta Shida /matatizo katika Maisha yako ..
YESU Kristo amesimama mlangoni ( Kwenye familia yako ,Moyo wako katika ya Ukoo na ndugu zako ikiwa utaruhusu aingie mahali hapo atafanya mabadiliko yake juu ya watu wote na kila jambo lililopo mahali hapo ..
IPO milango mingi lakini sisi tunayo mamlaka ya Ya kufungua na kufunga hiyo milango
Mathayo 16:19 " Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni."
Yesu Kristo ametupa funguo za mamlaka ya Ufalme wa Mhinguni ambazo zinatusaidia sisi kufunga na kufungua milango ya Shida mbalimbali katika Maisha yetu.
AINA YA UFUNGUO
1:UFUNGUO WA TOBA.
Rejea 2 Nyakati 7:14
ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.
Toba inabadilisha uchumi na tabia ya mtu binafsi na nchi kwa Ujumla.
Toba inafanya tuombe na kusikilizwa na Mungu. .
Inatufanya tuache njia mbaya ..
Inatufanya tusamehewe dhambi zetu.
2Wakorintho 10:4
4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo.
Tunaangusha ngome kwa kuomba Toba
Ukitenda dhambi itakupeleka utumwani ,Mfano Magonjwa ,Uchumi kuyumba ,ulevi
Ili Mungu ajibu maombi yetu lazima akusamehe kwanza.
Toba /Kutubu ni kuomba msamaha kwa Mungu na kuonesha kwamba unahitaji msaada wa Mungu
Yeremia 29:1 Maneno haya ndiyo maneno ya waraka, ambao nabii Yeremia aliupeleka toka Yerusalemu, kwa hao waliobaki wa wakuu waliochukuliwa mateka, na kwa makuhani, na kwa manabii, na kwa watu wote, ambao Nebukadreza aliwachukua mateka toka Yerusalemu hata Babeli.
Mungu akubariki kwa somo hili fupi
Zawadi Ngailo
P.o box 124
Sikonge TABORA
+2556231 32 195
MAISHA NA NENO LA MUNGU
No comments:
Post a Comment