Wakolosai 1: 15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.
18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote.
19 Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;
20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.
21 Na ninyi, mliokuwa hapo kwanza mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha sasa;
22 katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele zake, watakatifu, wasio na mawaa wala lawama;
23 mkidumu tu katika ile imani, hali mmewekwa juu ya msingi, mkawa imara; msipogeuzwa na kuliacha tumaini la Injili mliyosikia habari zake, iliyohubiriwa katika viumbe vyote vilivyo chini ya mbingu; ambayo mimi Paulo nalikuwa mhudumu wake.
¶Yesu Kristo siyo kiumbe kama nusu Malaika Bali ni
Mungu mwenyewe .
¶Mungu haonekani lakini tunaweza kumuona na kumjua kwa njia ya Yesu Kristo .
Yesu ni Mungu na hivyo hakuumbwa..
Alikuwepo kabla ya kuumbwa vitu vyote
Ni mkuu kuliko viumbe vyote.
Yeye mwenyewe ni Muumbaji ..
Ni asili na mtawala wa Vitu vyote ..
Vinavyoonekana na visivyoonekana pamoja na Ulimwengu wote wa Kiroho yaani wa viumbe wa Malaika
¶Yesu Kristo ni kusudi na lengo la viumbe vyote
Viumbe vyote vipo kwa ajili ya Utukufu wake (16-17)
Yesu Kristo ana uungu wa milele ndani yake unaomfanya kuwa asili na kichwa cha Viumbe vyote vionekanavyo .
Yesu Kristo ni asili na kichwa cha Uumbaji mpya yaani Kanisa kwa sababu ya USHINDI WA UFUFUO WAKE .
YESU KRISTO ni mtawala mkuu ..Hana mchanganyiko wa Mungu na Malaika Bali katika nafsi yake mwenyewe ana hali kamili na Uwezo wa Uungu ( 18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote.
19 Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;)
Yesu Kristo ni mpatanishi wa wenye dhambi ..Kwa njia ya kifo chake watu tunarudishwa katika hali ya Amani na mapatano na Mungu (Verse 20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni).
Sisi kama wakristo kama ilivyokuwa kwa wakolosai walivyoona /tulivyoona nguvu ya Mungu katika maisha yao /yetu tumeokolewa katika dhambi zetu .
Wokovu wetu umetokana na Kristo mwenyewe aliyefanyika mwanadamu mwenye mwili kama sisi naye amezichukua dhambi zetu nasi tumewekwa huru mbali na dhambi na hukumu ya Milele .
Nguvu ya malaika ama mwanadamu au kitu chochote haziwezi kuongeza jambo lolote katika hayo yaliyofanywa na Kristo .
21 Na ninyi, mliokuwa hapo kwanza mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha sasa;
22 katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele zake, watakatifu, wasio na mawaa wala lawama;
23 mkidumu tu katika ile imani, hali mmewekwa juu ya msingi, mkawa imara; msipogeuzwa na kuliacha tumaini la Injili mliyosikia habari zake, iliyohubiriwa katika viumbe vyote vilivyo chini ya mbingu; ambayo mimi Paulo nalikuwa mhudumu wake.
Ili tuweze kusimama mbele za Mungu katika ukamilifu wa Kristo ni lazima tushikamane sana na ukweli wa Kristo..
Tunapaswa kutambua kwamba kazi ya Kristo imekamilika ..
Ukweli wake upo katika msingi wa Injili mahali popote injili inapohubiriwa wala haiwezi kubadilishwa ili ifae kwa mawazo Fulani za kibinadamu ...
Yesu Kristo ni yeye yule Jana leo na hata milele .
Mungu akubariki kwa Ujumbe huu mfupi Jumapili ya Leo
Na
Zawadi Ngailo
Sikonge Tabora
©2017
Contact
. http://ishineno.blogspot.com/
https://m.facebook.com/maishaneno/
https://m.facebook.com/groups/166019753924509?view=permalink&id=226923244500826
http://zawadingailomedia.blogspot.com
https://m.facebook.com/zawadifngailo/
No comments:
Post a Comment