Tuesday, January 24, 2017
Jifunze kuishi maisha ya kusamehe
Katika maisha tunayoishi Hapa Duniani kwakuwa tu wapitaji basi na makwazo hayana budi kutokea ila tunajifunza, kama vile ambavyo mtu Mwema anavyoweza kujifunza ubaya akawa Mtu muovu ndivyo ambavyo mtu mubaya anavyoweza kujifunza wema na akawa mtu mwema inategemea unajifunza kwa nani, kwa Mungu au kwa Shetani
Mwenye sifa ya kusamehe dhambi Maandiko yameweka wazi ni Yesu kristo peke yake hivyo ni Vema tukajifunza kwake,
Mathayo 11:29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.
Ø Utu wema
Ø Upole
Ø Unyenyekevu wa Moyo
Ø Kupata raha nasfsini tunajifunza kwa Yesu kristo,
Ø Mungu anataka ujifunze leo itakusaidika ikiwa utakuwa tayari kujifunza,
Ø utayari wako ni wa muhimu Sana ruhusu mabadiliko yaanzie kwako,leo
Watu wengi sana wanaokosewa Wanasamehe sana lakini kusahau tukio au kwazo lililosababisha msaha utoke ni vigumu sana kusahau, Na hili ndilo jambo linalowatesa kila inapoitwa leo, kutosahau kosa baada ya kusamehe nikuendelea kuutunza Ugonjwa badala ya kutibu, Hata kanuni ya Mungu anaanza kutusamehe kabla hajatuponya magonywa yetu,
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment