Tuesday, January 24, 2017

MAISHA NA NENO LA MUNGU

Acha Neno la Mungu Liangaze Barabara Yako “Neno lako ni . . . nuru kwa barabara yangu.”—ZABURI 119:105. 1, 2. Ni katika hali gani neno la Yehova litaangaza barabara yetu? NENO la Yehova litaangaza barabara yetu tukiliruhusu lifanye hivyo. Ili kunufaika na nuru hiyo ya kiroho, lazima tujifunze kwa bidii na kufuata shauri la Neno la Mungu lililoandikwa. Hilo tu ndilo litakalotuwezesha kuwa na hisia kama hizi za mtunga-zaburi: “Neno lako ni taa ya mguu wangu, na nuru kwa barabara yangu.”—Zaburi 119:105. 2 Sasa tuzungumzie Zaburi 119:89-176. Mistari hiyo ina habari nyingi sana zilizopangwa katika beti 11, nayo inaweza kutusaidia kudumu katika barabara inayoongoza kwenye uzima wa milele.—Mathayo 7:13, 14. Kwa Nini Ulipende Neno la Mungu? 3. Zaburi 119:89, 90 inaonyeshaje kwamba tunaweza kulitegemea neno la Mungu? 3 Tukilipenda neno la Yehova tutakuwa imara kiroho. (Zaburi 119:89-96) Mtunga-zaburi aliimba: “Mpaka wakati usio na kipimo, Ee Yehova, neno lako limesimama mbinguni. . . . Umeiweka dunia imara, ili ipate kuendelea kusimama.” (Zaburi 119:89, 90) Kwa neno la Mungu, yaani, ‘sheria zake za mbingu,’ jua, mwezi, na nyota husonga katika mizunguko yake pasipo kugongana, nayo dunia imewekwa imara milele. (Ayubu 38:31-33; Zaburi 104:5) Tunaweza kulitegemea kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova kwa sababu kila asemalo “hakika litafanikiwa” katika kutimizwa kwa kusudi lake.—Isaya 55:8-11.

No comments:

Post a Comment