Tuesday, January 24, 2017

JIFUNZE KUSAMEHE NA KUSAHAU

Yeremia 1:4  Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.  Tangu tumboni Mwa mama mzazi  ndipo tunapoanzia kujifunza Mambo mbali mbali,kwa kuhisi hali ya mazingira tunayotarajia kuja kuishi,  Tunapofika ulimwenguni tunaendelea kujifunza kwakuhisi,kuona,kusikia, kila kitu, kutofautisha ni pale utapopata Neema ya Mungu kwakuwa tunaishi katika falme mbili, unapokuwa bado tumboni unaishi katika falme tatu, Mungu,mzazi,shetani japo falme kuu bado inabaki kuwa ya Mungu Falme kuu mbili  zinazofanya kazi hapa Duniani, Ø  Ufalme wa Mungu- (Nuru) Ø  Ufalme wa Muovu-(Giza) Ni vizuri ukafahamu hilo kwanza kabla ya mengineyo Mengi ,Ufalme wa Mungu Unasimamiwa na Mungu Mwenyewe Katika Utatu Mtakatifu Mungu Baba,Mwana,na Roho Mtakatifu, katika mambo yote matakatifu, Ufalme wa Muovu (Shetani)nao unasimamiwa na Shetani mwenyewe na majeshi yake,Katika mambo maovu yote, Falme hizi zote zina fanya kazi katika Ulimwengu wa ki-Roho na kujidhihirisha katika Ulimwengu unaoonekana kwa Macho ya Damu na nyama, kwa sababu Maalumu, na Hizi falume zinashindana kila wakati,  Waefeso 6:12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. Mema yote au Mabaya yote  yanafanyika kupitia Falme hizi nilizozitaja hapo juu, Mwanadamu asipotumika katika Mema basi atatumika katika Mabaya,asipomtumikia Mungu atatumikishwa na Shetani, usiposababisha makwazo utasababishiwa,

No comments:

Post a Comment