Sunday, September 10, 2017

UKOMBOZI


1 Yohana 1:7 bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.

Tunapoenenda katika nuru tunashirikiana na Kristo
Palipo na nuru Macho huo vizuri ..Ukitembea Nuruni huwezi kujikwaaa

a) Damu ya Kristo ni Upatanisho

Damu inapatanisha ..Tumetenganishwa na Dhambi lakini Damu ya Yesu imetupatanisha na Mungu /,kutoka katika dhambi.

Wakosai 1:20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.

       Kwa Damu ya Yesu tumekombolewa ..
       
Damu lazima isafishe dhambi zote..

Ufunuo 7:13 Akajibu mmoja wa wale wazee akiniambia, Je! Watu hawa waliovikwa mavazi meupe ni akina nani? Na wametoka wapi?
14 Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe. Akaniambia, Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya.

     Kanisa lazima Liwe Takatifu ..

Aliyeshinda dhambi ndio mshindi wa kuingia Mbinguni ..

Damu ya Yesu imekuja kututengeneza ..

Damu ya Yesu ipo kwa ajili ya Mtenda dhambi

Ipo kwa ajili ya MAISHA yetu.

Unapoaasi dhbi inakupata ..

Ni wakati wa kuutazama Msalaba  wa Yesu ..

Bila kuwagiwa kwa Damu Kristo tiungeangamia

Waebrania : Mlango 13

12 Kwa ajili hii Yesu naye, ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa nje ya lango.

       Damu ni upatanisho wa nafasi zetu na Mungu..

Walawi 17 :11 Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.

Tunamshinda Shetani kwa njia ya Damu ya Yesu Kristo peke yake.
    
Ufunuo 12:
11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

Friday, September 8, 2017

MADHABAHU

MADHABAHU ni mahali rasmi ambapo watu au mtu hutumia kufanya ibada kwa Mungu au mungu ambaye ndiye mwabudiwa. Kuna utofauti kati ya mungu wa herufi ndongo na Mungu huyu wa herufi kubwa ya mwanzo , huyu ni mungu wa dunia hii ambaye hakuumba mbingu na nchi ,ila Mungu wa herufi kubwa ya mwanzo huyu ndiye Mungu muumbaji.
Kutoka 20:2-3 ‘‘Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miung mingine ila mimi. ”
MUHIMU: usitumie herufi ndogo mwanzoni unapo andika kumwakilisha Mungu wa muumbaji, ni kosa kubwa sana.
IBADA HUJUMUISHA YAFUATAYO; Kuadhimisha, kutoa sifa , kutoa sadaka ,kuomba na kumtumikia Mungu au mungu.
Ndipo akasimama Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zake makuhani , na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na ndugu zake, nao wakaijenga madhabahu ya Mungu wa Israel, ili kutoa sadaka za kuteketezwa juu yake, kama ilivyo andikwa katika toati ya Musa , mtu wa Mungu. Ezra 3:2
AINA ZA MADHABA
(i) Madhabahu ya Mungu wa mbinguni.
Je Baba yetu Ibrahimu hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipomtoa Isaka mwanawe juu ya madhabahu.Yakobo 2:21.
Hii ni madhabahu ya kweli ambayo ndiyo iliyo sahii kwa mtu aliye mwamini Yesu kuijua kwa undani zaidi.
(ii) Madhabahu za kishetani. Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene , katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari mambo ya dini. Kwasababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya Ibada yenu, naliona madhabahu iliyo andikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYE JULIKANA. Basi mimi nawahubiri habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua. Matendo 17:22-23.
Ni dhahiri kwamba mtume paul aliyo iyona ni madhabahu ya kishetani ambayo ipo kinyume na mapenzi ya Mungu wa Kweli. Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.1korintho10:14-22. Ibada ya sanamu ni ipi? ni ibada inayo fanywa kwa mungu wa dunia hii, ambaye ni shetani.
HIZI NI BAADHI YA MADHABAHU ZA KISHETANI.
(a) Madhabahu za maji. Unaweza kuwa shahidi katika jambo hili yapo baadhi ya makabila ndani ya Nchi hii ya Tanzania na nchi nyingi duniani. Ambao hufanyia baadhi ya Ibada kwenye mito, baharini, maziwa na mabwawa katika maeneo haya watu huenda kutoa sadaka, au huita kutambika. Tambua maji yanasikia kwahiyo upo uhusiano mkubwa katika ulimwengu wa roho kati ya maneno yanayo tamkwa kipindi cha kutoa sadaka. Tusome 2wafalme 2:19-22 Watu wa mji wakamwambia Elisha, Angalia, twakusihi, mahali pa mji huu ni pazuri, kama Bwana wangu aonavyo; lakini maji yake hayafai, na nchi huzaa mapooza. Akaseme,Nileteeni chombo kipya, mtie chumvi ndani yake. Wakamletea. Akatoka akaenda mpaka chemchemi ya maji, akatupa ile chumvi humo ndani, akasema, BWANA asema hivi, Nimeyaponya maji haya; hakutatoka huko tena kufa wala kuzaa mapooza. Hivyo yale maji yakapona hata leo, sawasawa na neno la Elisha alilolinena.
(b) Misitu na miti mikubwa. hii pia hutumika kama maeneo ya kufanyia Ibada za kishetani ambazo huusisha utoaji wa sadaka.
(c) Njia panda. Hili si geni kwa watu wengi katika miji na vijiji pia limekuwa likifanywa , kwa kutumia njia panda kama sehemu ya kutoa sadaka mbalimbali mfano; Nazi kuvunjwa, vibuyu kuvunjwa.
(d) Nguzo maalumu na minara. Haya yote yamekuwa maeneo ya kutolea sadaka katika miji mikubwa ambayo hasa vizazi na vizazi hulithi utamaduni huu.
(e) Milima. hasa milima mirefu hutumika kama maeneo muhimu katika Ibada za kishetani, na tambua kwamba tunapo ongelea ibada, Hakuna ibada pasipo kutoa sadaka. Swali ni kwamba sadaka hiyo inatolewa kwa nani ?
(f) Madhabahu za mateso.
Hizi humilikiwa na watu mfano, Wachawi, Waganga, Wanajimu na makuhani wa sanamu, hawa wote wanakuwa na kibali cha kipepo katika kuendesha ibada hizo ila kwa lengo la kutesa maisha ya watu tu.
Kazi yao ni kutengeneza Madhabahu hizo kwa ajili ya kupeleka Nguo, Majina, Picha,Vitu ,Fedha na visanamu vya watu wanaotaka wawatese. sababu hii hupelekea watumishi wa Mungu kuwafundisha sana, wakristo kuwa makini katika maisha yako ya kila siku ,una kula nini? Una vaa nini? Una ongea nini? yote haya katika ulimwengu wa roho yana umuhimu na yanaweza kumuonganisha mkristo hata yeye pasipo kujua.
Pamoja na kuangalia mfumo wa madhabahu za kishetani iko nguvu zaidi kwa madhabahu ya Mungu wa mbinguni. Mfano Elia na manabii. 1Wafalme 18:30-35, Jitahidi sana kuisoma habari hii yote na utaona jinsi ambavyo madhabahu ya ki-Mungu ilivyo na nguvu , ambazo ziliweza kumdhihirisha kuwa yeye ni Mungu mkuu.
MUHIMU: pasipo madhabahu hakuna msingi imara wa kiroho.
FAHAMU HATUA ZA KUJENGA MADHABAHU.
Jambo la kwanza fahamu ,Madhabahu zote za ki-Mungu lazima ziungamanishwe na kanisa lililopo hapa duniani.
Madhabahu yaweza kuwa ya mtu mmoja au kikundi cha watu wengi.
Mfano, Agano la kale Ezra 3:5 walitumia hasa kuchinja wanyama , ila kwa Agano jipya utaratibu hasa sa ni sadaka pasipo damu ya wanyama. Ila unaweza toa ; Pesa ,mnyama au kitu chochote
FAIDA YA MADHABAHU YA KI- MUNGU
(i) Huweka upatanisho (msingi)
Madhabahu ya ki-Mungu pale mwamini anapotoa sadaka, jambo la kwanza ni “UPATANISHO”
Mwanzo 18:6-10 ili Upatanisho uwe dhahiri ni endapo tu kutoa kutakuwa kwa moyo wa kupenda. Mfano unapo soma maandiko hayo yanaonyesha Baba wa Imani akifanya kwa kupenda na si kulazimiswa na watu, Ibrahimu alijua siri.
Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia , Ee Ibrahimu, Naye akasema , Mimi hapa. Akasema, umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye , Isaka , ukaende zako mpaka nchi ya moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu yam mlima mmojawapo nitakaokuambia. Ibrahimu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa. Mwanzo 22:1-3.
Kiukweli si kwamba Ibrahimu jambo hili katika hali ya kibinadamu lilikuwa lahisi kwake, ila mtumishi wa MUNGU huyu alijua maana ya madhabahu, Madhabahu unapo jenga huanzia rohoni kwanza kwahiyo pale alipo kubali kumtoa Isaka Kuwa sadaka ya kuteketezwa tayari alikuwa amejenga.
MUHIMU: Kwa kila jimbo, ulifanyalo kuwa makini katika kujenga Madhabahu.
(ii) Hufungulia Baraka.
Kupitia Madhabahu ya Mungu wa Israel, inaleta baraka za haki isivyo kawaida.
Ukisoma, Mwanzo 22:15-18 ''Malaika wa BWANA akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni. akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee, katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao; na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.''
Katika maisha yako ya kawaida jitahidi kabla ya kuomba Baraka, fanya kitu kwanza mbele za Mungu.
Soma maneno haya pia utaona jinsi Mungu anavyo toa maagizo kwa balaamu kuwa akanene na Baraki.Hesabu 23:16-20
Jitahidi upitie vifungu hivi pia vitakavyo kujenga sana juu ya baraka za KiMungu.
''na Baraka hizi zote zitakujulia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani'' Kumb 28; 2, 8.
''Atawabarikia wamchao BWANA, Wadogo kwa wa kubwa.'' zaburi 115:13
Atukuzwe Mungu , Baba wa Bwana wetu Yesu kristo, aliyetubariki kwa Baraka zote za rohoni , katika ulimwengu wa roho, ndani yake kristo. Efe 1:3
MUHIMU: tambua mambo ya rohoni huzaa na baadaye huja ya kimwili. Galatia 3:9 Unapofanya jambo hili Imani huitajika sana.
Tulio mwamini Yesu, wote tumebarikiwa ili kuzifanya Baraka ziwe dhahiri maishani mwako LAZIMA UFANYE KITU. Matendo ya mitume 3:25-26. ''Ninyi mmekuwa watoto wa Manabii na wa maagano yale, ambayo Mungu aliagana na Baba zenu, akimwambia Ibrahimu, katika uzao wako kabila zote za ulimwengu zitabarikiwa.''
(iii) Ulinzi wa Ki-Mungu.

Tambua Mungu wetu ni Mungu wa Maagano huachilia ulinzi katika maisha ya mtu kwasababu pale anapo mtazama mtu huyo huona “AGANO”. Mfano, ukisoma mandiko haya yote yanazidi kuonyesha faida ya maagano. Nuhu, Mwanzo 6:18, 9:11. ''Lakini nitafanya agano langu nawe kuwa thabiti; nawe utaingia katika safina, wewe na wanao, na mkeo na wake za wanao, pamoja nawe. na agano langu nitalithibitisha nanyi, wala kila chenye mwili hakitafutwa tena kwa maji ya gharika; wala hakutakuwa tena gharika , baada ya hayo, kuiharibu nchi.''
Maandiko yote haya yanaonyesha kuwa kupitia sadaka huweka agano ambalo Mungu huliangalia hilo kwa kipindi kirefu sana.
Ibrahimu, Mwanzo 17:4 ''mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi.'' Mungu wetu ni Mungu wa Maagano yeye huweka na hilo agano hudumu kwa kipindi kirefu sana, unapo toa sadaka inakuwa agano mbele za Mungu ambalo hudumu kwa kipindi kirefu sana.
Kumb 29:25 ‘‘Ndipo watakaposema watu, ni kwa kuwa waliacha agano la BWANA, Mungu wa baba zao, alilofanya nao hapo alipowatoa katika nchi ya Misri’’.
(iv) Humkumbusha Mungu. Jambo hili ni siri kubwa sana, Madhabahu huongea yaani Inasema mbele za Mungu. Zaburi 106:45 ''Akawakumbukia agano lake ; Akawahurumia kwa wingi wa fadhiri zake.''
Ufunuo 16:7a.''Nikasikia hiyo madhabah ikisema'' Kwahiyo katika maisha ukiwa kama mwamini unapo kuwa na tabia ya kujenga madhabahu kwa mambo uyafanyayo ,kwasababu kutokana na shughuri mbalimbali za kimaisha upo wakati utasahau wewe binafsi kama ulifanya kitu mbele za Mungu, ila Hiyo Madhabahu “ITASEMA MBELE ZA MUNGU KWAAJILI YAKO”
(V) Humdhiirisha Mungu au humfunua. 1wafalme 18:22, 32-38 ukisoma vizuri na kwa umakini utagundua kuwa ugomvi au ubishani uliokuwepo kati ya nabii Eliya na Manabii wa Baali ulikuwa nani Mungu wa kweli kati ya Mungu wa Eliya na wao Baali, ubishano wao ulikuwa mkubwa sana ambao usingwezwa kuisha kwa uhalaka kwasababu IMANI ni kitu cha thamani kwa mtu aliye nacho ,pale anapo amini juu ya jambo fulani si kwa ulahisi unaweza mwambia usiamini, ni mpaka pale UDHIHIRISHO unapo tokea. Kwahiyo Nabii Eliya akawaambia ‘‘kwa hiyo na watutolee ng’ombe wawili; wao na wajichagulie ng’ombe mmoja, wamkate-kate na kumweka juu ya kuni, wasitie moto chini; nami nitamtengeza ng’ombe wa pili, na kumweka juu ya kuni,wala sitatia moto chini. Nanyi ombeni kwa jina la mungu wenu, nami nitaomba kwa jina la bwana; na Mungu yule ajibuye kwa moto, na awe ndiye Mungu”.
Kiukweli katika maneno hayo, kinacho tamkwa ni kwamba LEO NA TUONE NANI ALIYE WA KWELI KATI YA mungu au MUNGU.
KITU CHA KUFANYA
Kama hukuwahi kujenga madhabahu jitahidi kujitoa kwanza kwa kujengea vitu vyako vyote ukianzia ,watoto wako, ndugu kiujumla. elimu ,biashara ili uviungamanishe na Mungu, pia baada ya kuyajua yote haya ,JITAHIDI UYAFANYIE KAZI NA MUNGU WA MBINGUNI AKUBARIKI.

Wednesday, September 6, 2017

KUBEBEANA MIZIGO

.          ”Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri Zake.”_ (Danieli 9:3, 4).*

Akiwa na mzigo kwa niaba ya Israeli, Danieli alijifunza upya unabii wa Yeremia. Ulikuwa waziwazi kiasi ambacho kwenye vitabu alielewa shuhuda hizi zilizorekodiwa “hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.”

Kwa imani ambayo msingi wake ulikuwa kwenye neno la unabii lililo imara zaidi, Danieli alimsihi Bwana kwa ajili ya kutimizwa upesi kwa unabii huu. Alisihi kwa ajili ya heshima ya Mungu kudumishwa. Katika ombi lake alijiweka yeye mwenyewe kikamilifu pamoja na wale waliokuwa wamepungua katika makusudi ya Mungu, akiungama dhambi zao kana kwamba ni zake mwenyewe.

Ombi lililotoka kwenye midomo ya Danieli lilikuwa la ajabu sana! Linadhihirisha nafsi iliyonyenyekea kiasi cha ajabu! Joto la moto wa kimbingu lilitambulika katika maneno yaliyokuwa yakipanda juu kwa Mungu. Mbingu ilijibu ombi lile kwa kumtuma mjumbe wake kwa Danieli. Katika siku zetu hizi, sala zinazowasilishwa namna hiyo zitashinda pamoja na Mungu. “Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana.”

Kama ilivyokuwa nyakati za kale, ombi lilipotolewa, moto ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kafara iliyokuwa juu ya madhabahu; hivyo, kama majibu kwa ajili ya maombi yetu, moto wa kimbingu utakuja kwenye roho zetu. Nuru na uwezo wa Roho Mtakatifu vitakuwa vyetu. Je, sisi hatuna hitaji kubwa la kumwita Mungu kama alivyokuwa Danieli? Ninanena na wale wanaoamini kwamba tunaishi kwenye kipindi cha mwisho kabisa cha historia ya dunia hii. Ninawasihi mbebe mioyoni mwenu mzigo kwa ajili ya makanisa yetu, shule zetu na taasisi zetu.

Mungu yule aliyesikia maombi ya Danieli atasikia maombi yetu tunapomjia kwa moyo wa toba. Mahitaji yetu ni ya muhimu pia, matatizo yetu ni makubwa na tunahitaji kuwa na makusudi yenye mkazo uleule, na kwa imani tumtwike mzigo wetu yeye aliye Mbeba-mizigo mkuu. Lipo hitaji kwa ajili ya mioyo kuguswa sana wakati wetu kama ilivyokuwa wakati Danieli alipoomba.

Tuesday, September 5, 2017

FAHARI YA KIJANA NI NGUVU ZAKO

Bwana Yesu Kristo atukuzwe wana wa Mungu aliye hai.
Ninazidi kumshuru Mungu kwa ulinzi wake na kuzidi kutukutanisha tena, jina la Bwana lihimidiwe.

Karibu sana mpendwa tusemezane katika ujumbe huu wa neno la Mungu ambao Roho wa Mungu ametupatia.

Ujumbe:FAHARI YA KIJANA NI NGUVU ZAKO.
               ======================

Katiika ujumbe wetu naomba kuzungumza na kusemezana na vijana wote wa kike na wa kiume,na labda Roho wa Mungu atasema nawe hata kama sio kijana basi naomba ulipokee neno hilo litakusaidia.

         Tusome MITHALI 20:29

Fahari ya kijana ni nguvu zao;Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.

Nguvu
---------- Ni uwezo unaomsababisha mtu kufanya jambo Fulani katika maisha yake.

➡Hizo nguvu ambazo unazo wewe kijana,naomba nikuambie kwamba Mungu hajakupa nguvu hizo kwa ajili ya:
👉Kuiba,kubaka,kubomoa nyumba za watu,wala hujapewa nguvu hizo kwa ajili ya kupiga watu,wala sio za kutukana wazee mitaani.

👉Bali  Mungu amekupa nguvu hizo kwa ajili ya kumtumikia,kwa ajili ya kufanya kazi nzuri za mikono yako naye akubariki,kwa ajili ya kuwasaidia wengine mpendwa.
➡Hivyo Tumia nguvu ulizonazo leo kumtumikia Mungu wako kijana wangu.

👉Lakini vijana wengi Leo tunazitumia hizo nguvu zetu vibaya sana nakuambia mpendwa; wengine wanazitumia kuvuta madawa ya kulevya,wengine kuiba,wengine kubaka mitaani,wengine kupigana,wengine kutukana watu.

➡Nakuambia wewe kijana utumiaye nguvu zako vibaya wakati wa ujana wako,nakuambia siku inakuja ambayo utazitafuta nguvu hizo.
➡Wengine husema siwezi kumtumikia Mungu nikiwa kijana,Bali nitamtumikia Mungu nikiwa mzee,hivi calender ya maisha yako unayo wewe mikononi mwako?.

      Soma hii hapa MHUBIRI 12:1-2

1⃣Mkumbuke muumba wako siku za ujana wako,Kabla hazijaja siku zilizo mbaya,Wala haijakaribia miaka utakaposema,Mimi sina furaha katika hiyo.

2⃣Kabla jua,Na nuru na mwezi,na Nyota havijatiwa Giza;Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;....

👉Unaona hapo 👆wewe kijana mwenzangu;neno linakuambia tumkumbuke Muumba wetu ambaye ni Mungu wetu katika siku za ujana wetu,kumbuka  kumtumikia BWANA Eee kijana .
➡Nakushangaa wewe unayesema kwamba unasubiri uwe mzee ndio utamtumikia Mungu.

👉Siku zinakuja wewe kijana ambazo hizo nguvu zako unazoziaribu Leo utazitafuta nakuambia.
➡Mungu anataka tumtumikie Maishani mwetu tukiwa bado tuna nguvu wapendwa.
➡Usisubiri umekuwa mgonjwa ndio sasa unakumbuka Mungu yupo,jitambue bado usiku haujakufikia mpendwa.

👉Acha kutumia nguvu zako kuwatukana wazee nakuambia kijana mwenzangu.Wewe ujajivunia huo ujana wako na kuanza kuwadharua na kuwatukana wazee,nakuambia huyo mzee unayemtukana na kumdharau alikuwa kijana kama wewe.

👉Yaani kinywa chako kimejaa matusi,maneno machafu dhidi ya wazee,nakuambia ole kwako.
➡Unajivunia nguvu zako kwa kuvuta bangi,naomba nikuambie kwamba hata na huyo mzee nguvu alikuwa nazo.

Wahenga walisema kwamba:
➡Kuishi kwingi ni kuona mengi√.
Sasa wewe huyo mzee unayemdharau alishayaona mengi sana,je utaomba ushauri kwake? Muheshimu mzee mpendwa kijana.

➡Tambua kwamba Wewe sio wa kwanza kuwa kijana,wapo waliokutangulia wewe ambao waliwaheshimu wazee wao na maisha yao yakawa mazuri sana,na Mungu akawafanikisha na kuwainua zaidi.

      Ona vijana hawa:

👉Kijana Yoshua alimuheshimu sana Musa,na baada ya kifo cha Musa Mungu akamuinua Yeye.

👉Kijana Samweli alimuheshimu sana Eli na akawa kijiana mwenye maadili mema,na Mungu akamtumia zaidi.

👉Kijana Timotheo alimuheshimu Paulo.
Na wengine wengi mpendwa ambao waliwaheshimu wazee wao;waliyasikiliza mausi,ushauri na maonyo yao, na Mungu akawainua zaidi na zaidi;kwanini wewe unamdharau mzee huyo?

👉Ni kweli kwamba Mungu ameiweka huduma kubwa ndani yako,lakini tambua unahitaji ushauri wa wazee ili uzidi kusonga mbele zaidi;acha kuwadharau na kuwatukana ewe kijana mwenzangu.

Jambo la kusikitisha ni kwamba:

➡Vijana wengi makanisani wakiinuliwa kihuduma,basi wanasema yatosha.

~Wakisomea Biblia na kupata diploma, degree, masters ya teologia basi wanajiona kwamba wamemaliza yote.

👉Wakijuwa kuimba,kupiga guitar basi wanasema yatosha.Wala hawapendi kuomba ushauri kwa wazee,mzee akimshauri utasikia wewe mzee wakati wako umekwisha,tuachie vijana.
➡Ni kweli wakati wake umekwishapita lakini sikiliza ushauri,Maonyo yake akuambiayo.
Ewe kijana nakushauri kwa huruma zake Mungu acha kumdharau mzee,Bali muheshimu sana maana huyo ni adhina kubwa kwako mpendwa.

             1TIMOTHEO 4:11-12.

👉Mambo hayo uyaagize na kuyafundisha.

👉Mtu awayeyote asidharau ujana wako,Bali uwe kielelezo kwao waaminio,katika usemi na mwenendo,na katika upendo na imani na usafi.

➡Lakini vijana wengi tunadharaulisha ujana wetu kwa matendo yetu mabaya katika jamii,ndimi zetu zimejaa matusi tuuuu,hivi kwa mwenendo wako huo utakuwaje kielelezo kwa watu? Jirekebishe kijana mwenye tabia mbovu na mbaya,la sivyo utaeendelea kuudharaisha ujana wako,na imani yako inakuwa sio kitu.

➡Acha kuudharaulisha ujana wako wewe kijana mwenzangu.
Na wewe mzee wangu kichwa chako kinathamani kubwa sana endapo kitaonekana katika njia bora ambayo inampendeza Mungu, usiwe wewe mwenyewe ndio chanzo cha kujidharaulisha mbele ya vijana,vijana tunahitaji maonyo yako,tunahitaji ushauri wako ili tusonge mbele zaidi,hivyo thamanisha uzee wako lakini pia thaminisha kichwa chako chenye mvi.Wewe ni adhina kubwa kwetu sisi vijana,jitambue nakuambia.

👉Vijana wenzangu naomba niwashauri kwamba Tusiwaige wale vijana waliomdhiaki Mtumishi wa Mungu Elisha,hatimaye wakaliwa na Dubu;Bali tuwaige wale vijana waliomuinua Musa mikono yake; Tuishi pamoja na wazee wetu,tutachota mambo makubwa kutoka kwao.

➡Ushirika wetu na wazee nakuambia utakufanya uonekane kuwa ni kijana unayeifahaa jamaa ya waaminio na hata wasioamini pia,kwa mwenendo wako safi nakuambia utawavuta wengine kuja kwa Yesu Kristo ya kuziokoa nafsi zao na mauti.
~Tukae bega kwa Bega na wazee wetu Mungu atatufanikisha na kutuinua zaidi wapendwa.

➡Tusiwadharau wazee,tuwaheshimu sana,tuombe ushauri kwa wazee ndugu zangu Mungu atatufanikisha.
➡Tumia nguvu zako vema mpendwa maana nguvu zako ndio fahari yako.

👉Thamani ya ujana wako iko mikononi mwako,thamani ya UJANA wako ni nguvu zako, Tumia Nguvu zako vizuri.
➡Usitarajie kuheshimiwa kama wewe mwenyewe hujajiheshimu mpendwa.
➡Thaminisha,Heshimisha ujana wako ewe kijana mwenzangu.

👉Kijana Mungu anahitaji umtumikie siku za ujana wako mpendwa, kabla hazijaja siku mbaya kwako.
➡Chunguza Sana ujana  wako leo.
➡Unaandikiwa  wewe kijana Maana unazo nguvu, na NENO la BWANA linakaa ndani yako. Nawe utamshinda huyu shetani kwa nguvu za NENO La Mungu ndani yako.

👉Kijana Jaza NENO la Mungu moyoni mwako nalo NENO litakuongoza Katika njia ikupasayo.

Saturday, September 2, 2017

UKUU WA KRISTO NA KAZI ZAKE

      Wakolosai 1: 15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.
18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote.
19 Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;
20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni.
21 Na ninyi, mliokuwa hapo kwanza mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha sasa;
22 katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele zake, watakatifu, wasio na mawaa wala lawama;
23 mkidumu tu katika ile imani, hali mmewekwa juu ya msingi, mkawa imara; msipogeuzwa na kuliacha tumaini la Injili mliyosikia habari zake, iliyohubiriwa katika viumbe vyote vilivyo chini ya mbingu; ambayo mimi Paulo nalikuwa mhudumu wake.

        ¶Yesu Kristo siyo kiumbe kama nusu Malaika Bali ni
Mungu mwenyewe .

    ¶Mungu haonekani lakini tunaweza kumuona na kumjua kwa njia ya Yesu Kristo .

Yesu ni Mungu na hivyo hakuumbwa..

Alikuwepo kabla ya kuumbwa vitu vyote

Ni mkuu kuliko viumbe vyote.

Yeye mwenyewe ni Muumbaji ..

Ni  asili na mtawala wa Vitu vyote ..

Vinavyoonekana na visivyoonekana pamoja na Ulimwengu wote  wa  Kiroho yaani wa  viumbe wa Malaika

¶Yesu Kristo ni  kusudi na lengo la  viumbe vyote

Viumbe vyote vipo kwa ajili ya Utukufu wake (16-17)

            Yesu Kristo ana uungu wa  milele ndani yake  unaomfanya kuwa asili na kichwa cha Viumbe vyote vionekanavyo .

       Yesu Kristo ni  asili na kichwa cha Uumbaji mpya yaani Kanisa kwa sababu ya USHINDI WA UFUFUO WAKE .

       YESU KRISTO ni  mtawala mkuu ..Hana mchanganyiko wa  Mungu na Malaika Bali katika nafsi yake  mwenyewe ana hali  kamili na Uwezo wa  Uungu ( 18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote.
19 Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae;)

       
         Yesu Kristo ni  mpatanishi wa wenye dhambi ..Kwa njia ya kifo chake watu tunarudishwa katika hali ya Amani na mapatano na Mungu (Verse 20 na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni).

       Sisi kama wakristo kama ilivyokuwa kwa wakolosai walivyoona /tulivyoona nguvu ya Mungu katika maisha yao /yetu  tumeokolewa katika dhambi zetu .

Wokovu wetu umetokana na Kristo mwenyewe aliyefanyika mwanadamu mwenye mwili kama sisi naye  amezichukua dhambi zetu nasi tumewekwa huru  mbali na dhambi na hukumu ya Milele .

       Nguvu ya malaika ama mwanadamu au kitu chochote haziwezi kuongeza jambo lolote katika hayo yaliyofanywa na Kristo .
21 Na ninyi, mliokuwa hapo kwanza mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya, amewapatanisha sasa;
22 katika mwili wa nyama yake, kwa kufa kwake, ili awalete ninyi mbele zake, watakatifu, wasio na mawaa wala lawama;
23 mkidumu tu katika ile imani, hali mmewekwa juu ya msingi, mkawa imara; msipogeuzwa na kuliacha tumaini la Injili mliyosikia habari zake, iliyohubiriwa katika viumbe vyote vilivyo chini ya mbingu; ambayo mimi Paulo nalikuwa mhudumu wake.

      Ili  tuweze kusimama mbele za Mungu katika ukamilifu wa  Kristo ni  lazima tushikamane sana na ukweli wa Kristo..

   Tunapaswa kutambua kwamba kazi ya Kristo imekamilika ..

Ukweli wake upo  katika msingi wa Injili mahali popote injili inapohubiriwa wala haiwezi kubadilishwa ili ifae kwa mawazo Fulani za kibinadamu ...

     Yesu Kristo ni  yeye yule Jana leo na hata  milele .

Mungu akubariki kwa Ujumbe huu mfupi  Jumapili ya Leo

Na

Zawadi Ngailo

Sikonge Tabora

©2017
Contact
. http://ishineno.blogspot.com/

       https://m.facebook.com/maishaneno/

https://m.facebook.com/groups/166019753924509?view=permalink&id=226923244500826

http://zawadingailomedia.blogspot.com

https://m.facebook.com/zawadifngailo/

Friday, September 1, 2017

ARISE AND PRAY

"I am the LORD thy God, which brought thee out of the land of Egypt: open thy mouth wide, and I will fill it. (Psa 81:10)

IF ONLY YOU WOULD PRAY

Result Oriented Prayers

Rest Orchestrating Prayers

Reproach Overcoming Prayers

Real Offensive Prayers

Record Opening Prayers
Resistance Obviating Prayers

Revelation Obtaining Prayers
Rapid Outcome Prayers

Relevant On-point Prayers

Regular Obligatory Prayers...

New Things Would Begin In Your Life.

Arise And Pray.

            

SOMO :TENGENEZA MLANGO WA MUNGU KUINGIA KWENYE SHIDA YAKO

         BWANA YESU ASIFIWE
Mpendwa Zipo shida nyingi sana katika Maisha yetu ambazo mlango wake wa kutokea ni YESU Kristo peke yake
       Kitabu cha Ufunuo 3:20 kinasema hivi .."
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

       YESU Kristo anasema tazama Nasimama mlangoni ,Nabisha ,MTU akisikia sauti Yangu na kuufungua mlango ,Nitaingia kwake nami nitakula pamoja naye ,Na yeye pamoja nami .

            Mlango waweza kuwa ni moyo wako ,Mwili wako waweza kuwa mlango ,Familia ,Ukoo na ndugu zako vinaweza kuwa Mlango wa kuleta Shida /matatizo katika Maisha yako ..

                YESU Kristo amesimama mlangoni ( Kwenye familia yako ,Moyo wako katika ya Ukoo na ndugu zako ikiwa utaruhusu aingie mahali hapo atafanya mabadiliko yake juu ya watu wote na kila jambo lililopo mahali hapo ..

          IPO milango mingi lakini sisi tunayo mamlaka ya Ya kufungua na kufunga hiyo milango

Mathayo 16:19 " Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni."

      Yesu Kristo ametupa funguo za  mamlaka ya Ufalme wa Mhinguni ambazo zinatusaidia sisi kufunga na kufungua milango ya Shida mbalimbali katika Maisha yetu.

AINA YA UFUNGUO

1:UFUNGUO WA TOBA.

Rejea 2 Nyakati 7:14
ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.

      Toba inabadilisha uchumi na tabia ya mtu binafsi na nchi kwa Ujumla.
  Toba inafanya  tuombe na kusikilizwa na Mungu. .

Inatufanya tuache njia mbaya ..

Inatufanya tusamehewe dhambi zetu.

2Wakorintho 10:4
4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo.

   Tunaangusha ngome kwa kuomba Toba

Ukitenda dhambi itakupeleka utumwani ,Mfano Magonjwa ,Uchumi kuyumba  ,ulevi

       Ili Mungu ajibu maombi yetu lazima akusamehe kwanza.

Toba /Kutubu ni kuomba msamaha kwa Mungu na kuonesha kwamba unahitaji msaada wa Mungu

Yeremia 29:1 Maneno haya ndiyo maneno ya waraka, ambao nabii Yeremia aliupeleka toka Yerusalemu, kwa hao waliobaki wa wakuu waliochukuliwa mateka, na kwa makuhani, na kwa manabii, na kwa watu wote, ambao Nebukadreza aliwachukua mateka toka Yerusalemu hata Babeli.

Mungu akubariki kwa somo hili fupi

Zawadi Ngailo
P.o box 124

Sikonge TABORA

+2556231 32 195

MAISHA NA NENO LA MUNGU

   
   

KIOO CHA NG'AMBO

KIOO CHA NG'AMBO

Matendo 28:3

[3]Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni, na kuuweka motoni, nyoka akatoka kwa ajili ya ule moto akamzonga-zonga mkononi.

Moto pekee ndio unaweza kutoa nyoka aliye katikati ya kuni

Naamini una mipango mizuri pamoja na maamuzi mema juu ya jambo fulani, lakini katika mipango na maamuzi hayo kuna nyoka(maumivu) ndani yake

Neno la Mungu(Moto) ndilo linaweza kupima uzuri wa maamuzi na mipango yako na kuondoa nyoka(maumivu) ndani yake

Mipango na maamuzi yako yasipite neno la Mungu(1wakor 4:6)

Ubarikiwe. ...

Na Tuvuke Mpaka Ng'ambo

Friday, July 14, 2017

MAPAMBO

Wana wa Mungu,Bwana Yesu Kristo asifiwe.Habari za uzima wapendwa.
Ni matumaini yangu kwamba wewe ni mzima wa afya tele katika Bwana.

Nakukaribisha mpendwa tusemezane  na tujifunze neno la Mungu.

            Ujumbe: M A P A M B O
                         ===============

Tutambue kwamba kuna aina mbalimbali  za mapambo wapendwa.
Leo nakuletea hizi hapa.

Neno Mapambo
-------------------------: Ni jumla ya urembo uliyowekwa ili kupendezesaha mwili au sehemu yoyote ile,au kupendezesha kitu Fulani.

Aina ya Pili ya Mapambo
-------------------------------------: Ni fedha au Mali inayolipwa na mwanaume kwa wazazi wa mwanamke anayetaka kumwoa,yaani mahari.

Lakini neno Pambo
-----------------------------Ni kitu cha kupendezesha au kitu cha kuongeza uzuri;kitu cha kupendezesha mahali Fulani.
Sisi tunakwenda kuzungumzia hiyo aina ya kwanza.

Baada ya kuyaona maneno haya,mpendwa tutambue kwamba katika ulimwengu wa Leo kuna aina nyingi sana za mapambo ambazo zinapamba na kupendezesha sshemu mbalimbali ya mazingira yetu,lakini pia yapo mapambo kwa ajili ya kuupendezesha mwili wa mwanadamu.

~Katika ujumbe huu napenda kuzungumza na nyie wanawake  mnaoipamba miili yenu kwa mavazi ya aibu ili ipendeze .
√ Sio kwamba wanaume hawavai vibaya Hapana ; bali leo Roho wa Bwana ameniongoza kusema nanyi akina mama.

Mimi binafsi nawatia moyo na kuwapongeza wanawake wote kwa habari kujipamba,nakuambia hivi jipambe sana tu ; lakini ni mapambo yapi ujipambe  ?  Fuatana nami.

~Katika dunia hii ya Leo najua kuna aina nyingi za saloon zenye hadhi mbalimbali na zina wataalamu wa viwango vya juu sana na wa tofauti tofauti;katika saloon hizo wanawake hutumia gharama nyingi sana ambazo zinawachukulia sehemu ya maisha yao.
~Saloon hizi zinabadirisha ngozi,shepu na hata miundo mbalimbali ya mapambo na wengine hujipamba hadi kupitiliza kiasi.Nakuambia wakina mama wanatumia gharama kubwa saba na wengine hata kugombana na waume zao pindi wakikosa kupewa hela ya kwenda saloon, wengine huenda mbali na kutafuta wanaume wa nje ya ndoa.

~Lakini nimegundua saloon moja,ambayo haitaji kuharibu pesa yako,wala kutafuta awara,wala kugharamikia kitu chochote kama unataka kupambwa.

    Sikiliza hii mpendwa 👂👂

👉 Siku moja nilikuwa napita mahali Fulani,nikaona akina mama Fulani wanaingia katika saloon moja hivi ya kifahari sana ili kwenda kujipamba wapendeze,mkononi mwangu nilikuwa na Saloon nzuri sana nakuambia we acha tu,saloon hii ikikupamba mpendwa kila mmoja atakupenda tu,utakuwa nuru gizani,utakuwa msaada wa walio wengi.
Na Saloon hii niliokuwa nayo si kitu kingine Bali nilikuwa na Biblia mkononi mwangu.

~Nilipowaona wale akina mama nikatamani niwashauri waje kwenye hii saloon niliyokuwa nayo ili wajipambe na wapambwe na wapendeze sana.Mpendwa nakuambia hivi Saloon hii haipo mbali na wala hauhitaji gharama nyingi bali gharama yako ni kuiamini na kuikubali biblia isemavyo.
~Basi nikaenda kuwaambia wale akina mama: Naomba mnisikilize kidogo,wakasema Hakuna shida mtumishi.
~Kwakuwa nilikuwa tayari nimejuwa wapi wanaenda na kufanya nini, nikawaambia Jamani Mimi ninayo Saloon nzuri sana hapa ambayo haihitaji gharama kama huko Mwendako.
~Wakasema Saloon hiyo iko wapi ili tusigharamikie?
Nikawaambia Saloon yangu ni BIBLIA hii tu.
~Wale akina mama walishtuka sana kusikia vile, walinishangaa sana ; nikawaambia msishituke naamini mtanielewa tu.

Niawaambia Hivi wewe mama Unakubalije kukaa bila kujipamba na wakati Biblia imekurusu?.
~Wakaniambia Kwanini umesema hivyo?

Nikawaambia tusome:
        1PETRO 3:5

√ Ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani,waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao√.

Wale akina mama washangaa,wakaniuliza mtumishi Wanawake wa zamani walijipambaje?

Nikawaambia na kuwajibu 👇

   Tusome 1PETRO 3:3-4

3 Kujipamba kwenu,kusiwe kujipamba kwa nje,yaani,kusuka nywele,na kutia dhahabu,na kuvaa mavazi;

4 Bali kuwe utu wa moyoni usioonekana,katika mapambo yasiyoharibika;Yaani,roho ya upole,na utulivu,iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.√

Hivyo nikawaambia enyi akina mama kwa mujibu wa Biblia kujipamba kwenu sio kwa nje Bali ni kwa ndani ya mioyo yenu.
Yaani muwe na roho ya utulivu,roho upole ndani yenu kwa mapambo haya hayaribiki kamwe.
~Wale akina mama wakaelewa,Uamuzi ukawa kwao kuifuata biblia au kuikataa;Mimi nikaondoka zangu.

Ewe mpendwa msikilizaji na msomaji wangu tunakiona na kugundua hapa ni kwamba:

~roho ya upole ni pambo.
~roho ya utulivu ni pambo.
Lakini pia mpendwa tujuwe kwamba:
~roho ya uvumilivu ni pambo.
~roho ya utu wema ni pambo.Na mengine mengi.

Mpendwa mapambo haya ni adimu sana kwa wanawake wa siku za Leo.Mapambo haya hayapatikani katika saloon yoyote ile hapa duniani,Bali yanapatikana Ndani ya Biblia tu.

✍ Ili ujuwe kuwa mtu ana roho ya utulivu ni pale yanapotokea machafuko na misukosuko.√
~Ukimuona mwanamke unatokea msukosuko kidogo  ndani yake,halafu anaenda kumtangaza mumewe nje ya ndoa yake, tambua ya kwamba huyo hajapambwa,hana ya uvumilivu na utulivu.
~Ili ujuwe mwanamke ana roho ya upole ndani Yake, ni pale inapotokea fujo, kelele,vurugu ndani ya ndoa yaani hapo utamtambua tu.
~Wanawake wengine wanakosa pambo la upole kiasi kwamba mumewe hatamani kurudi mapema nyumbani.

👉 Leo hii utakutana na mwanamke mkristo,lakini alivyojipamba sasa utaogopa kumwangalia Mara mbili;yaani inatia aibu jamani.
~Utamkuta amevaa kinguo kifupi sana,tena kimebana mwili wake, mapaja nusu utupu.
~Wengine wanavaa magauni mepesiiiii,wengine vitaiti na vipedo.
Ukimuangalia kichwani jamani ni hatari sana nakuambia, shedo utafikiri ameweka maji midomoni,wanja nayo, mmmmm....alafu hapo anasema biblia imeruhusu tujipambe.
~Na kanisani wanaingia,kukaa inakuwa shida,na watumishi tunakaa kimya tu.
Wengine mnatembea nusu uchi,nguo za ndani zikionekana,ramani ya.... Yote inaonekana.Jamani mnatutia aibu mjuwe.
~Ni kweli biblia imeruhusu ujipambe,lakini mapambo ya ndani yaani jipambe kwa roho ya upole,utulivu,uvumilivu,utu wema... Sio hayo mapambo ya mwili wako.

Wanawake jamani jipambeni kwa mapambo ya  ndani jamani,ni mapambo yasiyoharibika Bali yanadumu milele,hata ukinyeshewa na nvua hayatoki ndani yako. Jipambeni mwenendo safi na tabia njema ili muwavute maana hivyo ndivyo walivyojipamba wenzenu wa kale.

                👇👇

✍ Jipambeni Kwa roho ya Upole.

✍ Jipambeni kwa utu wema ndani ya mioyo yenu.

✍ Jipambeni kwa moyo wa utulivu.

✍ Jipambeni kwa mwenendo na  tabia njema .

✍ Jipambeni kwa adabu nzuri

Hujakatazwa kujipamba Ewe Binti yangu, ewe mama yangu Hujakatazwa kujipamba ; lakini jipambe kwa mambo tajwa hapo juu👆.
✅ Kwasababu mambo hayo hayaaribiki kamwe hata inyeshe Mvua kiasi gani.
-Ujisipambe kwa mavazi au Kwa dhahabu au Kwa lulu mwilini kwako ; bali Vaa mavazi ya Heshima, Mavazi ya Kuusitiri mwili wako.
✍ Achana Na hivyo vipedo, Vigauni Vifupi vyenye kuonyesha mapaja yako.

✍ Achana Na visiketi vifupi, Achana Na blouse zenye kuacha matiti yako nje nje jamani kwa maana hayo yanakudhalilisha ,yanaishusha thamani ya mwili wako, lakini pia yanaudharaulisha Wokovu wako ewe  Mama Na binti yangu katika Kristo.

√ Binti na  Mama yangu katika Kristo, Tunza thamani ya mwili wako ; heshimisha mwili. wako kila uendako ; huwezi kumuhubiria Mtu mmwingine Injili  ya Bwana Yesu Kristo Huku umevaa nusu uchi. √

Saturday, April 29, 2017

MADHARA YA KUKOSA MAARIFA YA MUNGU

MADHARA YA KUKOSA AU KUONDOLEWA KWA MAARIFA YA MUNGU KATIKA MAISHA YAKO

LUKA 11:52

52 Ole wenu, enyi wana-sheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa maarifa; wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia.

BWANA YESU APEWE SIFA SANA SANA

Neno ole ni neno linaloashiria kuwepo kwa madhara juu hilo lililofanyika au fanywa

Wanasheria wa Musa walijikuta wanaingiza sheria ambazo azitoi maarifa kwa watu juu ya kumjua Mungu wao ,waliweka maarifa ambayo hayakuwafanya wajue ukweli juu ya Mungu wao badala yake wakawa wanaondoa hali ya kuwafanya wawe karibu na makini na  kweli ya neno la Mungu ,waliondoa njia ya kupata maarifa ya kumjua Mungu wao lakini pia sheria hizo hizo ziliwaharibu na wao pia walipozisikia ,maana ziliondoa maarifa ya kumjua Mungu kwa watu na kwao pia ,kwahiyo ziliwafunga wote watungaji na wasikiaji pia

Ukisoma ile Danieli  1:1-5 ,Mfalme Nebukadreza alijitafutia vijana wenye maarifa ni mmoja wa vijana aliowachagua wasimame mbele zake kutoka katika taifa la Israeli Daniel alikuwa n mmoja wapo kabisa sasa angalia ile Daniel 6:1-17👉�Utaona kuwa mawaziri na maliwali waliona wivu juu ya Danieli na wakamtafutia mashitaka ili kumvuruga katika maisha yake na ili kumvuruga walitaka kutumia sheria ya Mungu wake ,na sheria ya Mungu ni utaratibu wa Mungu juu ya mtu ambao uwa unamfanya yule mtu kumjua na kumuelewa Mungu wake na kufanya yampendezayo kwahiyo wakaona kuwa ili kumkosesha lazima tuingize sheria ambazo zitamfunga katika kumjua na kumfuata Mungu wake maana waliona chanzo cha mafanikio yake n maarifa au ufahamu alionao ndani yake juu ya Mungu wake ivyo wakabadili sheria ya nchi na katika hiyo sheria wakaweka na kipengele cha kumfungia Danieli asiweze kuendelea kumtafuta Mungu wake arudi nyuma na kumkosea Mungu wake lakin Danieli alikataa kukaa katika hiyo sheria kabisa na Mungu alimpigania ,unakuta mtu yuko kanisani alafu ghafula mambo yanabadilika pale anaona watu wamemuinukia au kama hawampendi anarudi nyuma au mapito yamekuwa magumu juu yake anarudi nyuma na kuhacha kumtafuta Mungu na wokovu anahacha ,ndugu hapo unakuwa unaondoa ufunguo wa maarifa mwenyewe ,Danieli aligoma akaendelea na Mungu wake ,hakuacha maarifa ya kuendelea kumuomba Mungu ,aliendelea na Mungu akampigania hakuondoa ufunguo wa maarifa kwa sababu ya sheria ya mawaziri na wakubwa

Swala la kuombea sheria zinazotungwa juu ya nchi n muhimu sana kwa sababu ujui n kipengele gani kitakubana na kukuondolea maarifa ya Mungu wako ,kule marekani kipengele cha kuruhusi ushoga na usagaji kwenye sheria yao kimeondoa maarifa ya kumjua,kumuhofu ,kumuheshimu ,kumpenda Mungu kabisa ,ufunguo uo mbaya wa sheria umewafungia wengi kumjua Mungu na kumuishia Mungu na ubaya wa sheria hizo uwezi kutunga na kuzipitisha bila ya kwanza kukuathiri na wewe mtungaji lazima wapitishaji wawe nao wao wanafanya hayo ya makufuru kwa Mungu na hata kwa Danieli wale waliotunga ile sheria juu ya Danieli waliingia kwenye moto wenyewe

Hosea 4:6-9

"Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa ;kwakuwa wewe umeyakataa maarifa ,mimi nami nitakukataa wewe ,usiwe kuhani kwangu mimi ;kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako ,mimi nami nitawasahau watoto wako "

Sheria ya Mungu wako yaani ule utaratibu wa Mungu wako uo ndio wenye kufungua maarifa ya Mungu maishani mwako ,ukikosa huo sahau kuwa na maarifa ya Mungu na maangamizi yatakuwa juu yako

Ndio maana tunashauriwa tujae maneno ya Mungu ndani yetu na yakijaa yatatupa kujua Mungu wetu anataka nini na yukoje na hatutaweza kuangamia kabisa

Ukisoma ile 1Wakor12:4-12

Liko neno la maarifa ambalo uwa linaleta maarifa kwa watu wa Mungu na hilo neno linahachiwa kwetu kama tukikaa katika kumpendeza Roho Mt ,anatupa ili litupe maarifa ndani yetu na kujua namna ya kuenenda na la kufanya mbele za Mungua

Monday, April 3, 2017

JINSI YA KUSHINDA KUKATA TAMAA

Jinsi Ya Kushinda Kukata Tamaa

Halipo jambo moja pekee unaloweza kulifanya sikuzote kwa sababu kama tulivyokwisha kuona, sababu za kukata tamaa hazifanani. Lakini zifuatazo ni baadhi ya hatua unazoweza kuchukua:

Watambue Wababe Walioko Langoni
Wababe wawili wanaolinda lango la kuingilia kwenye nchi ya ahadi hata leo wanaitwa hofu na kukata tamaa. Ikiwa sasa unasikia sauti zao, na kuhisi msukumo wa ushawishi wao, basi ujue kwamba upo karibu sana na ahadi zako.
Katika kipindi hiki muhimu, kama ilivyokuwa kwa Yoshua, unapaswa kuwa hodari na moyo wa ushujaa na kusonga mbele katika neema anayokupa Mungu (Yos 1:9).
 
Elewa Kinachoendelea
Katika 2Kor 4:16,17 Paulo anasema tusilegee kwa sababu kwa kupitia dhiki yetu utu wetu wa ndani unafanywa upya. Anasema dhiki yetu nyepesi na iliyo ya muda mfupi tu, inatufanyia kitu chema katika Mungu.
 
Tumaini Kwa Mungu
Hata kama imani yako ni ndogo, bado unaweza kumtumaini Mungu na kuamini kwamba Mungu wa amani atamseta Shetani mara chini ya miguu yako (Zab 42:5) (Rum 16:20).
 
Kiri Hitaji Lako, Mshirikishe Mwenzako Kisha Mwombe
Katika Mhu 4:12 tunaona kwamba uwezo wa watu wawili ni mkubwa kuliko wa mtu mmoja. Usihifadhi tu mawazo yako, mshirikishe mwenzako na halafu mwombe pamoja, na kumfunga Shetani.
 
Pokea Kutoka Kwa Mungu
Fungua moyo wako na umwachie Roho Mtakatifu akuhudumie kwa habari ya saburi na faraja ya Mungu, tumaini, furaha na amani (Rum 15:5, 13).
 
Shughulikia Sababu Za Asili
Wakati Eliya alipokuwa amechoka na kukata tamaa, Mungu alimpelekea chakula na pumziko kabla hajashughulika na sababu zenyewe na kumpa neno jipya, mwelekeo mpya, na tumaini jipya (1Fal 19:3-18).
 
Simama Kwenye Ahadi Ya Mungu
Petro anatuasa kuwa wanyenyekevu chini ya mkono wenye nguvu wa Mungu, kumtwika Yeye fadhaa zetu, kuwa na kiasi, kumpinga Shetani na kuwasaidia wengine wanaoteseka. Anatupa tumaini kubwa kwa kusema kwamba Mungu wa neema yote atatujia mara ili kututengeneza, kututhibitisha na kututia nguvu (1Pet 5:6-11).
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE UTUKUFU WA BWANA.

BY STELLA MBOGELA

Sunday, March 26, 2017

SHALOM

Bwana Yesu asifiwe milele!
Leo nataka nianze kukufundisha juu ya: “Mambo unayohitaji kuyajua kuhusu ndoto unazoota ili iwe vyepesi kufanikiwa kimaisha”.
Jambo la 1: “Usiipuuzie ndoto uliyoota hata ikiwa hukijui chanzo cha ndoto hiyo!”
Mfano wa Kwanza: Unaposoma kitabu cha Mwanzo 41:1 – 7, unaona ndoto mbili alizoota Farao, kwa usiku mmoja, na kwa kufuatana. Ndoto zile mbili zilikuwa na tafsiri moja iliyofanana. Na zilikuwa na ujumbe mmoja uliofanana, uliokuwa unamjulisha ujio wa njaa nchini Misri miaka 7 baadaye – tokea wakati ule alipoota zile ndoto.
Farao alipoamka alijisemea moyoni mwake ya kuwa: “Kumbe ni ndoto tu” (Mwanzo 41:7). Hii ikiwa na maana ya kwamba wazo la kwanza lililomjia moyoni mwake, baada ya kuamka usiku ule, ni kuzipuuzia zile ndoto – na wala asiwe na mpango wa kuzifuatilia.
Lakini biblia inasema, “asubuhi roho yake ikafadhaika” (Mwanzo 41:8); ikiwa ni kiashiria chenye ujumbe toka kwa Roho Mtakatifu, kwamba asizipuuzie ndoto zile! Asante Yesu hakuzipuuzia, na akatafuta msaada, ili ajue tafsiri yake. Yusufu alimtafsiria zile ndoto na kumpa maelekezo yaliyoambatana na ndoto zile. Na Farao akatekeleza maelekezo aliyopewa. Na hata njaa ilipotokea miaka 7 baadaye haikuwasumbua – kwa kuwa ujumbe wa ndoto uliwapa kujiandaa.
Je, umewahi kujiuliza ingekuwaje kama Farao angezipuuzia zile ndoto? Ni dhahiri ya kwamba angezipuuzia – angeona tu baada ya miaka saba njaa kali yenye kudumu miaka saba – huku hajajiandaa nayo!Na kwa vile njaa ile ilikuwa ni ya “dunia yote” (Mwanzo 41:56,57), ina maana dunia yote ingekumbwa na njaa, kwa sababu tu ya Farao kuzipuuzia ndoto – ikiwa angeamua kuzipuuzia zile ndoto!
Mfano wa pili: Danieli 4:1 – 34 tunaelezwa madhara yaliyompata mfalme Nebukadreza, kwa sababu aliipuuzia ndoto aliyoota!
Ndoto ile – ilikuwa inampa onyo mfalme Nebukadreza, juu ya mwenendo wake aliokuwa nao wakati ule. Na ndoto ile ilimpa pia kujua adhabu atakayopewa asipobadili mwenendo wake. Lakini pia kwenye ndoto ile aliyoota, alipewa maelekezo ya mambo ya kufanya, ili aliyoyaona kwenye ndoto yasimpate – lakini alipuuzia! Soma Danieli 4:27. Tena – alipewa miezi 12 ya kujirekebisha – lakini alipuuzia – na wala hakuitumia nafasi hiyo – na matokeo yake yote aliyoyaona kwenye ndoto, yalimtokea katika maisha yake!Kwa kuipuuzia ile ndoto, Mfalme Nebukadreza aliingia kwenye adhabu ya maisha yake, na afya yake kuvurugika kwa nyakati saba au miaka 7! Na pia “nafasi” yake ilikosa uongozi kwa miaka 7!
Mfano wa tatu: Yusufu – yule aliyekuwa mume wa Mariamu, na mlezi wa Yesu wakati akiwa mtoto, aliota ndoto nne, ambazo angezipuuzia – historia ya ukristo isingekuwa ilivyo sasa!
Ndoto ya kwanza iliyoandikwa kwenye Mathayo 1:18 – 24 tunaona akihimizwa na “malaika wa Bwana”, kuwa asihofu kumchukua Mariamu akiwa na mimba. Na akajulishwa juu ya jina na kazi ya mtoto atakayezaliwa. Biblia inasema: “Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza;akamchukua mkewe” (Mathayo 1:24).
Ndoto ya pili iliyoandikwa kwenye Mathayo 2:13 – 18, Yusufu alionywa na Malaika wa Bwana, juu ya mipango ya mfalme Herode ya kutaka kumwua Yesu. Na akaelekezwa amchukue Yesu na mama yake awapeleke Misri – na akae kule Misri hadi malaika wa Bwana atakapompa maelekezo mengine!
Biblia inasema juu ya Yusufu baada ya kuota ndoto hiyo ya pili ya kuwa: “Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri” (Mathayo 2:14). Hata Herode alipotuma watu Bethlehemu kumtafuta Yesu na kumuua – wakakuta hayupo! Na kwa hasira aliua watoto wote wa kiume wa eneo lile; “tangu wenye miaka miwili na waliopungua” (Mathayo 2:16).
Ndoto ya tatu aliyoota Yusufu, iliyoandikwa katika Mathayo 2:19 – 21, ndiyo iliyomfanya aondoke Misri na familia yake, na kuanza kurudi nchini Israeli.
Ndoto ya nne aliyoota Yusufu, iliyoandikwa katika Mathayo 2:22 – 23, ndiyo iliyomfanya amchukue Yesu na mama yake, na kuwapeleka kuishi nao “katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazarayo” (Mathayo 2:23).
Huo ulikuwa ni utii wa hali ya juu sana kwa Yusufu! Hasa tukichukulia maanani ya kuwa Yesu hakuwa mtoto wake wa kumzaa; tena – maelezo ya kumtunza Yesu na hata kumwepusha na hatari zilizomkabili, alikuwa anapewa kwa njia ya ndoto – ambazo watu wengi wangeweza kuzipuuzia.
Lakini Yusufu hakuzipuuzia zile ndoto, na utii ule uliweka mwanzo mzuri wa Yesu, katika kumwandaa kwenye huduma, na kazi ya Mungu, aliyotumwa kuifanya duniani!
Je, wewe una kiwango gani cha utii kwa maelekezo ambayo Mungu anakuletea kwenye ndoto? Au kila ndoto unaipuuzia kama mfalme Nebukadreza? Je, unaweza ukapewa taarifa na Mungu kwa njia ya ndoto ukaielewa na kuitii?
Mtu mmoja aliyenisikiliza kwa njia ya redio tarehe 6 Nov, 2015, nikifundisha juu ya ndoto kwa kutumia biblia, alinitumia ujumbe ufuatao kwa njia ya simu:
“Bwana Yesu asifiwe – mwalimu! Mafundisho uliyotupa leo yamegusa maisha yangu, kwa sababu kuna ndoto niliota tarehe 24.12.2013 – sitaisahau siku hii! Niliota niko kijijini kwetu huko….napambana na nyoka. Huyo nyoka alikuwa amesimama usawa wangu – na akawa ananitishia kuning’ata. Na mimi nilikuwa namkemea kwa jina la Yesu. Lakini ghafla nikaona amenigonga, na kuniuma kwenye kidole cha pili cha mguu.
Ghafla nikashtuka toka usingizini. Nikakuta kidole kile alichonigonga na kuniuma yule nyoka katika ndoto, kinatoka damu na kinauma sana! Kulipokucha nikaenda kanisani kwetu, ambako siku hiyo kulikuwa na maombi ya kufunga. Mchungaji akawa anaombea wagonjwa. Akaniuliza unaumwa nini? Nikamjibu hivi: nimeota ndoto usiku …na kabla sijamaliza kujieleza nikaanguka.
Kuja kushtuka na kuamka, nikaambiwa nilikuwa na pepo mauti, ambaye waliweza kumkemea, na akaondoka toka mwilini mwangu.
Lakini tangu hapo maisha yangu yakayumba sana. Ijapokuwa nimeokoka…lakini sisongi mbele! Maisha yamekuwa magumu sana, na uchumi wangu umeyumba!Tena tangu siku hiyo niliyoota ndoto hii nilifukuzwa kwenye nyumba niliyokuwa nimepanga.Nikapanga nyumba nyingine – nayo pia tumefukuzwa mwezi wa sita mwaka huu”.

Mungu aendelee kukubariki sana!

Wednesday, March 22, 2017

NI SALAMA ROHONI MWANGU

*Shida isikutoe kwenye mstari*

Wimbo wa *Ni Salama Rohoni Mwangu* ulitokana na mikasa iliyomkuta  mwanasheria na wakili mahiri mkristo aliyeitwa Heratio Spafford.

Alikuwa na watoto watano akiwemo wa kiume mmoja. Mwanae pekee wa kiume alifariki mwaka 1871 akiwa na miaka minne.

Mwaka 1872 kulizuka moto mkubwa sana maarufu kama moto mkubwa wa Chicago ambao uliteketeza shamba na majumba yake, vitu alivyokuwa amejipatia kwa fedha alizoingiza kutokana na umahiri wake katika taaluma na kazi yake.

Mwaka 1873 alitanguliza  mkewe na mabinti zake wanne kwenda mapumziko Ulaya ambapo angewafuata kesho yake baada ya kumaliza kazi alizokuwa nazo.

Meli iliyokuwa ikiitwa Ss Ville du Havre iliyobeba familia yake ilizama na binti zake wote walifariki akapona mkewe tu ambaye alimtumia  telegramu *Nimepona mimi tu*.

Akiwa njiani kurudi nyumbani kwake nyumba ilimokuwa ofisi yake ikaungua. Kwa bahati nzuri nzuri alikuwa ameikatia bima lakini kampuni ya bima ilikataa kumlipa kwa madai kuwa lile lilikuwa  janga la asili (An Act of God).  Heratio alibaki mtupu - hana pa kuishi wala hana fedha. Akiwa ni mtu wa kiroho aliyemtegemea Mungu alikaa akitafakari yale yaliyokuwa yakitokea katika maisha yake na ndipo alipochukua kalamu na karatasi na kuandika *"Lolote liwalo, Bwana wangu, umenifundisha kusema - Ni salama rohoni mwangu*".  (Maandishi mengine yanasema aliandika maneno haya alipofika eneo la bahari ilipozama meli akiwa safarini kumfuata mkewe Ulaya). Baadae maneno haya yaliongezwa mashairi na kutiwa muziki na kuwa wimbo maarufu sana na wenye mguso wa kipekee wa *Salama Rohoni*. Kama ilivyokuwa kwa Ayubu Heratio alikuja kuinuliwa akapata watoto wengine na mali na fedha.

Mpendwa uliyefiwa, unayeuguza, unayeugua, uliyeishiwa, uliyevunjwa moyo, unayepitia tabu yoyote tukumbuke hakuna giza la kudumu. Tukumbuke Mungu yupo na ameahidi kumlinda kila amtazamaye asivunjwevunjwe au kufa moyo kutokana na taabu.

Kwa mfano huu wa Heratio tunajifunza kuwa ukubwa wa jaribu si tatizo bali mitazamo yetu kuhusu maisha. Ukipatwa na shida ufanye nini? Ujione hufai? Useme Mungu amekuacha? Useme shetani amekuinukia na amekushinda? Ujitoe uhai? Ulalame na kunung'unika usiku na mchana siku nenda rudi? La hasha! Kwanza ondoa tumaini lako kwenye vitu vya kupita na uweke tumaini lako kwa Mungu aliyeviumba na kukuumba. Nafsi yako imhimidi Mungu na kumshukuru kwani pamoja na shida yako kuwa nzito bado kuna vingi vya kumshukuru kwavyo. Hata hivyo atabaki kuwa Mungu. Huyu Mungu amesema katika mambo yote anakuwazia mema. Hata katika jambo baya kwako kuna jema analokuwazia ambalo wewe hulioni. Daudi alisema ajapopita katika bonde la uvuli wa mauti (shida, mateso, majaribu) hataogopa mabaya kwani anaamini katika gongo na fimbo ya Mungu. Akazidi kusema anataka neno moja tu kwa Bwana, nalo ndilo atakalolitafuta. Autazame uzuri wa Bwana na kutafakari hekaluni mwake. Hekaluni mwa Bwana ni kwenye moyo wako. Tafakari ukuu wa Mungu humo badala ya ukuu wa tatizo.

Iwe salama, salama moyoni mwako. Amen.

Monday, March 13, 2017

FAIDA ZA KUMTEGEMEA MUNGU!, Hakuna aliyemtegemea Mungu akapata hasara, ukimtegemea Mungu kuna faida, hebu angalia hizi faida za kumtegemea Mungu:-  (1)Bwana atakupa haja ya moyo wako->ZABURI 37:4.  (2)Kila ulitendalo litafanikiwa->ZABURI 1:3, MITHALI 3:5-6.  (3)Utakuwa na Amani->AYUBU 22:21.   (4)Mema yatakuijilia->AYUBU 22:21.  (5)Utabarikiwa->YEREMIA 17:7, ZABURI 112:3.  (6)Uzao wako utakuwa hodari->ZABURI 112:2.  (7)Utamwona Mungu ktk maisha yako->YOHANA 14:21, MITHALI 8:17.   (8)Mungu anaweka ulinzi juu ya maisha yako->ZABURI 34:7, MITHALI 3:21-26.  (9)Bwana atasikia kilio chako yaani maombi yako->ZABURI 34:15.  Kumtegemea Mungu ndio Maisha ya ushindi kwa mkristo, 

Wednesday, March 8, 2017

NGUZO YA SIKU

Zaburi 24:1
. Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake.

Zaburi 24:2
. Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari, Na juu ya mito ya maji aliithibitisha.

Zaburi 24:3
. Ni nani atakayepanda katika mlima wa Bwana? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?

Zaburi 24:4
. Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.

Zaburi 24:5
. Atapokea baraka kwa Bwana, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.

Zaburi 24:6
. Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.

Zaburi 24:7
. Inueni vichwa vyenu, enyi malango, Inukeni, enyi malango ya milele, Mfalme wa utukufu apate kuingia.

Zaburi 24:8
. Ni nani Mfalme wa utukufu? Bwana mwenye nguvu, hodari, Bwana hodari wa vita.

Zaburi 24:9
. Inueni vichwa vyenu, enyi malango, Naam, viinueni, enyi malango ya milele, Mfalme wa utukufu apate kuingia.

Zaburi 24:10
. Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Bwana wa majeshi, Yeye ndiye Mfalme wa utukufu. Kama TU MALI YA BWANA NA MALI, ELIMU NA CHOCHOTE ALICHONACHO MTU NI MALI YA BWANA, KWA SABABU HIYO BASI IMETUPASA KUWA TAYARI KUKABIDHI MIOYO YETU AITAWALE YESU, Niwatakie asubuhi njema

KUNYAMAZA

.CHAGUA KUNYAMAZA

MITHALI 11:
12 Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

MITHALI 17:
28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima;Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.

Changamoto kubwa tuliyonayo ni kwamba tunataka kuongea kila wakati, tunataka kujibu kila tunachokisikia, kila tunachokiona tunataka kukisemea kitu

Kuna wakati tunasikia na kukutana na mambo ambayo kiuhalisia moyo unagoma kabisa kunyamaza, unatamani ujibu, unatamani uwaambie watu yale umefanyiwa, unatamani uelezee vile umeumizwa lakini kumbe si kila jambo linatakiwa kuongelewa

Si kila ukionacho unatakiwa kukisemea kitu

Si kila usikiacho/uambiwacho ni lazima ujibu

Si kila ufanyiwacho ni lazima umwambie kila mtu

MUHUBIRI 3:
1 Kwa kila jambo kuna majira yake,Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;

Ipo nguvu katika kunyamaza

Yapo mambo ambayo tunapaswa kuongea, kusema, lakini yapo mambo ambayo tunapaswa kunyamaza kwaajili ya usalama wa Roho zetu

Ni kweli kuna wakati unasemwa sana vibaya, unasingiziwa, unatukanwa nk nk, lkn ni lazima ukumbuke kwamba kuna mazingira ambayo hupaswi kujibizana hata kama umeumia kiasi gani

Unajua ni kwanini?

Ukisemwa vibaya, ukitukanwa, ukidharauliwa lazima moyo utaghafirika, moyo ukighafirika lazima utakuwa na hasira na ghadhabu

Ukiwa na hasira katu usitegemee kuwa utajadiliana na mtu kwa hekima

Ukiongea utaongea katika uwepo wa hasira, ukijibu utajibu kulingana na kiwango cha hasira ulichonacho.

"AKUSHINDAE KUONGEA, MSHINDE KUNYAMAZA".....

HALELUYA

Shalom

*...Mkiisha kuwekwa  huru....*
       🌹lazima kuwa huru katika maisha yetu ili tuwe mbali na dhambi. 👇🏽👇🏽

*Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru, na kuwa mbali na dhambi, na kufanywa watumwa wa Mungu, mnayo faida yenu, ndiyo kutakaswa, na mwisho wake ni uzima wa milele. Warumi 6 :22*

      🙆🏽‍♂kumbe dhambi na kutokuwa huru kunatunyima kupata ya kutakaswa, na tena tunakoswa uzima wa milele.

       🙇🏽pia hakuna uzima wa milele bila utakaso, hivyo Tafuta utakaso upate uzima usio na mwisho. 😀😀

_usililie baraka ila Lilia utakaso kwanza_

       ©Mwl Erick Machumu
      0752763020

Sunday, March 5, 2017

TAFUTA AMANI NA MUNGU

Shalom KANISA

TAFUTA AMANI NA MUNGU
Mithali 8:17 "
Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. "
Isaiah 55:6
Mtafuteni Bwana, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu;
Waebrania 12:14
Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
Yohana 3:16
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
UNAPENDWA NA MUNGU!
Wewe ni wa thamani sana hata kama haujui! Mungu anakupenda! Alimtoa kristo akafa msalabani ili kulipa deni la dhambi zetu zote tulizofanya na kumwasi mungu kwani.Thamani ya ko ni Damu ya Mwana wa Mungu isiyo na ila wala dhambi...Halleluyah,Unapendwa!
1Peter 1:18-19 "18
"Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu;19 bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.
20 Naye amejulikana kweli tangu zamani, kabla haijawekwa misingi ya dunia; lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yenu; 21 ambao kwa yeye mmekuwa wenye kumwamini Mungu, aliyemfufua katika wafu akampa utukufu; hata imani yenu na tumaini lenu liwe kwa Mungu."
Umeamini? Unapendwa! Kristo alikuwepo miaka mingi mingi milele yote,lakini alifunuliwa kwajili yetu sote,mimi na wewe, sisi ni sababu hasa ya kristo kuja ulimwenguni. Unapendwa!
UNAMHITAJI YESU KRISTO,FANYA UAMUZI SASA UMKARIBISHE MAISHANI MWAKO.
Hizi ndio sababu kwa nini unamhitaji Yesu kristo:
Warumi 3:23 " kwa sababu wote wamefanya dhamb i, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;"
Warumi 5:12 Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;
Maandiko yanaendelea kueleza juu ya huyu Yesu kristo inasema katika
"Warumi 5:18-19
18 Basi tena, kama kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima. 19 Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki."
UNATAKIWA KUFANYA NINI?
Hebu tuone hapa jinsi maandiko yanavyotupa jibu:
Matendo ya mitume 2:37-40
"Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.
Matendo ya Mitume 16:30-31
" kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako."
Inawezekana nawe unajiuliza ya kwamba unawezaje kupokea kipawa hiki cha Mungu cha wokovu kwa njia ya Yesu Kristo ukisema na kuuliza moyoni
"Tutendeje, ndugu zetu?".Jibu linapatikana unatakiwa kufanya yafuatayo:
1.Tubu dhambi zako zote ulizotenda mbele ya Mungu kwa kumwambia kwamba umekosa na muombe akusamehe na akupe nguvu ya kushinda hiyo dhambi ili usije ukaanguka tena.atakusamehe na kukupokea ikiwa utafanya hivyo kwa moyo wako wote na kwa imani. Pia
"Mithali 28:13 Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema."
2.Mwamini Bwana Yesu na mkaribishe kwenye moyo wako na maisha yako. Ni Yesu pekee ndio mwokozi wa ulimwengu na hakuna njia nyingine yoyote ile ya kumfikia Mungu isipokuwa kristo Yesu hata anasema mwenyewe
"Yohana 14:6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. "
3.Liitie Jina la Yesu
Tunaokolewa kwa kupitia jina moja tu! vizazi vyote na jamii yote ya mwanadamu tunaokolewa kwa jina la yesu. JINA LA YESU NDILO LILILOBEBA WOKOVU WA KILA MWANADAMU
Imesemwa katika Mathayo 1:21 "Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao." pia anasema
Matendo ya Mitume 2:21 "Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa."
Warumi 10:13 " kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka."
Usiache nafasi hii ikupite bila ya kuliitia jina la Yesu hakika litafanya kazi kwako!
Liitie Jina la YESU KRISTO kwanjia ya maombi toka moyoni mwako na mwombe Bwana akusamehe dhambi zako zote nawe utaokoka sasa! hivyohivyo ulivyo Kristo anakupenda na kamwe hatakutupa ukimwendea.kwa ahadi hii hakikisha umefanya uamuzi wa kumpa kristo maisha yako .
Yohana 6:37
"Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe."
Yohana 6:35
"Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe."
Biblia katika Yohana 12:44-50 inasema:
"Naye Yesu akapaza sauti, akasema,
Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi bali yeye aliyenipeleka.45 Naye anitazamaye mimi amtazama yeye aliyenipeleka.
46 Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani. 47 Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu.
48 Yeye anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye; neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho. 49 Kwa sababu mimi sikunena kwa nafsi yangu tu; bali Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema.
50 Nami najua ya kuwa agizo lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo mimi, kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo.
Je nawewe ni miongoni ambao bado unamkataa YESU na maneno yake? lini utamkubali na kumwamini?.kumbuka YESU Ni MWOKOZI WAKO,AMEKUFIA MSALABANI na saa ya wokovu ni sasa FANYA MAAMUZI YA KUMFUATA KRISTO!.
Sali sala hii fupi toka moyoniUkimtazama na kuamini kwamba Mungu anakusikia kama umeamua kumwamini yesu na unataka atawale maishani mwako,akupe furaha amani na msamaha wa dhambi na akufanye kuwa mwana wa mungu sawasawa na alivyoahidi omba ukisema:
"BWANA YESU NINAKUJA KWAKO MIMI NI MWENYE DHAMBI NINAOMBA UNISAMEHE NA KUNIOKOA.KARIBU KWENYE MAISHA YANGU NA MOYO WANGU,UNISAMEHE MAOVU YANGU YOTE,UNIOSHE NA KUNITAKASA.KUANZIA SASA MIMI NI WAKO.NINAKUSHUKURU KWA KUWA ULIKUFA MSALABANI KWA AJILI YA DHAMBI ZANGU NA KWA KUNIPOKEA.SASA NIMEOKOKA.MIMI NI MWANA WA MUNGU,
Amen"
Sasa ndo umeokoka ivyo, Kristo ameingia ndani yako,wewe sasa umekuwa kiumbe kipya kwani anasema katika
"2Wakorintho 5:17
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya ; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. " pia ahadi hii inakuhusu sana anasema "
Yohana 1:12
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; "
Mambo ya kuzingatia:
1. Zungumza na Mungu kwa maombi kila siku (Yohana 15:7)
2. Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku (Matendo ya Mitume 17:11)
3. Mruhusu Roho Mtakatifu akutawale (Wagalatia 5:16-25; Warumi 8:14-17)
4. Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako (1Petro 5:7; Zekaria 4:6)
5. Usiache kukusanyika na kushirikiana na wengine waliompokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao kama wewe ili uimarike zaidi (Waebrania 10:25)
Unapendwa!
MUNGU wa mbinguni ni Baba yako.sema naye kwanjia ya maombi na sikia kutoka kwake kwanjia ya kusoma Biblia.Kama unapata shida.
Jenga mazoea ya Kusoma Biblia nakushauri anza na kitabu cha Yohana Mtakatifu,ukimaliza Soma Warumi halafu malizia Biblia yote katika hali ya maombi na kumwamini Mungu utashangaa kuona jinsi Mungu anavyokupenda na alivyo kuahidia mambo mazuri mno katika ulimwengu wa sasa na ule unaokuja baada ya kufa.Omba usiache.

LESSON THE POWER OF POSITIVE THINKING

Welcome to the Lesson : THE POWER OF POSITIVE THINKING. DON’T be discouraged! You WILL succeed!
It breaks my heart to see how many people today, especially young people, are ignoring God’s word or even turning their back on his word in order to pursue and fulfil what they call their ‘purpose’ or ‘destiny’ in life. They think they have to eat and drink from another source other than the word of God to get what they want, and the source they eat and drink at is the philosophy of this world, the ideas and thoughts of unbelievers, of those who don’t know God, who live independently of God and believe in their own ability and powers to fulfil their dreams and become successful. In this sense, they drink from a river the proceeds from the devil himself. They follow the teachings of atheists. The teaching arose in about the 1950s and although there are different variations of this teaching, they all come under the heading of ‘the power of positive thinking.’ Many popular preachers, who call themselves Christians, now promote these ideas, and those who are more interested in becoming successful in their careers and business than in following Jesus Christ eagerly absorb these teachings as though the Bible had never been written. What is the teaching of ‘the power of positive thinking’, what is the teaching of these people who totally disregard God? Well, I will quote some of their standard statements. it goes something like this:
‘Everything depends on your attitude. If you want to be successful you need to change your attitude. If you have the wrong attitude you will always be unsuccessful and poor. Change your thinking! Only think positively and you will succeed. Grasp the opportunity! Your future is in your hands; everything depends on the decisions you yourself make! Start thinking big, start dreaming big, start imagining big things for yourself! Have confidence in yourself! Persevere and in the end you will be victorious! Don’t give up! Never be discouraged! Pursue your dreams! The way to success is paved with failure, so don’t give up! Focus on those things that will help you to fulfil your destiny! Associate with those people and with those contacts who will help you achieve your dreams! You need to discover your purpose in life! How can you fulfil your destiny if you haven’t discovered your purpose in life? Your destiny is in your hands.’
What I have just quoted are some typical statements of those who promote the power of positive thinking, that is, just by having the ‘right’ attitude, you can be ‘successful’ and ‘fulfil your dreams’. This is the anti-Christian, or we can say, antichrist teaching of unbelievers who turn their backs on God and want to fulfil their own ambitions and dreams, believing it is their efforts and choices that will make them successful. It is amazing and distressing to see how many young Christians swallow this unbiblical self-centred approach. It is not God-centred, it is not Christ-centred, it puts you yourself in the centre! None of the above statements that I quoted f come rom the Bible or have anything to do with the Bible! Most quotes do not mention verses from the Bible. Although some of the words are similar to what we find in the Bible, nevertheless the context and the source from which they come are totally different – like a difference between light and darkness! All the statements lead you to put confidence in yourself, in your decisions, in your abilities, in your powers, while ignoring the God who gave His Son that you should be His and His alone!
Now of course, some of the statements above have a definite element of truth in them, JUST LIKE what the devil said to Eve had A DEFINITE ELEMENT OF TRUTH, when he told her that they would become as God if they ate from the tree of the knowledge of good and evil! And this part was true! Because after they had eaten that fruit, God said, ‘Behold, the MAN IS BECOME AS ONE OF US, to know good and evil.’ So the devil’s words had one aspect of truth, but it was not THE TRUTH, it was not the WHOLE truth, so it led them into sin, into independence from God and into SEPARATION from God. And this is what the teaching of the power of positive thinking will do in your life if you follow it.
One quote said that God blesses you only ‘spiritually’, but that YOU YOURSELF are responsible for making your life shine with success! Not only is such a thought unbiblical, it represents blasphemy against God! It is a slander against God. He knows if a sparrow falls to the ground, how much more does he not know about every step of your life and my life! God knows us through and through; he knows everything about us, from the time we get up to the time we go to bed! Do we really think that God has no interest in the choices we make; that God has no interest in the direction that our lives should take? Do we think that somehow we have to make choices independent of God in order for our destiny to be successful? Do we not read the Bible? Are we followers of Christ or not? In Ephesians chapter 2 and verse 10 it says this, ‘for we are HIS workmanship created in Christ Jesus unto good works which God has BEFORE ORDAINED that we should walk in them.’ Do we know this verse? Do we believe this word? Or do we feel safer if we take our lives out of the hands of God, out of his direction, and make our own decisions? Do we really think that by committing our lives to Christ and trusting him for every step we take that some how we will lose out, that we will miss our destiny? Is God in charge of our lives – yes or no?
It is clear from the posts many people put on Facebook that they do not know the Bible, that they are not lead by the word of God in their lives, that they do not understand the nature of God and who he is, and that they do not understand that they do not belong to themselves any more but to the one who loved them and died for them. How can we think that the only alternative to fulfilling our dreams and ambitions by our positive thinking, is to be left helpless, like a passive piece of wood in a river, being carried by life’s circumstances without direction, without destiny, without hope? How can Christians have an attitude like this? If we are talking about changing our attitudes in order to change our lives, THEN THIS FALSE ATTITUDE, this slander against God IS THE ATTITUDE THAT NEEDS CHANGING! Not to follow the anti-Christian teaching of the power of positive teaching DOES NOT MEAN that your life is left at the mercy of your circumstances! There is a God who loves you so much that he gave his Son to die for you, not just to forgive you, save you from sin and bless you with every spiritual blessing in the heavenlies, but He has a path and a way for you to walk in. Are you interested in his will for your life? Do you seek first his kingdom and righteousness? So why drink the poison from the river of the power of positive thinking? Are you afraid, are you really afraid, do you really believe that by trusting God, by putting your life in his hands, by committing to him every step that you take, that you will miss out on the things that God himself has prepared for you? Do you want God to ordain the steps you take or do you want to choose them yourself without reference to him? It gets to a point where I asked myself what is being preached in churches today, are young people really being converted and brought into this salvation that Christ died for?
Where does the Bible say ‘trust in yourself’, ‘have a positive attitude and you will succeed’, ‘changing your attitude is the secret to success’? WHY DO BELIEVERS NOT QUOTE THE BIBLE to encourage one another? I think the reason is this: the word of God does not give us the freedom to choose our own way, and that’s exactly what people want to do today, although they say they are followers of Christ. They follow the teaching of atheists through the following the teaching of the power of positive thinking so they can get what they really want while having the appearance of it being God’s will in their lives! Why do believers not quote one of the most important and encouraging verses in the whole Bible that relates to this subject? Namely, Proverbs chapter 3 verses five and six, which says, ‘trust in the Lord with all your heart and don’t lean to your own understanding. IN ALL YOUR WAYS ACKNOWLEDGE HIM AND HE WILL DIRECT YOUR PATHS.’ Why do they not quote this verse? I’ve not seen it anywhere on Facebook in reference to our future lives. Do they think God is not able to direct them, to fulfil HIS purposes for their lives? Is this what they think about God? Personally, I think part of the reason is this, that this verse, as with other verses in the Bible, bring God into the equation, bring God into the situation, bring God into your life! And then there is the fear that the things I personally really want may not come to pass! And that is the reason for the popularity of the teaching of the power of positive thinking! It puts the decision-making into your hands, not God’s!
Why don’t believers quote from Psalm 37 and verse five which says, ‘commit your way to the Lord, trust also in him, and he will bring it to pass.’ The idea that God can only bless us ‘spiritually’ but that we have to take over the direction of our lives by making our own choices, is a lie. Of course we have to think about things, of course we have to make decisions, of course there are opportunities that we need to consider! This is natural to life! This is not rocket science, this is no mystery! This is true of every person who has ever lived! THE QUESTION IS THIS, will you COMMIT your life, every step you take, every opportunity that comes along to the living God? This is the one issue! This is the heart of the matter! Committing every step we take, every decision we want to make into the hands of God does not deprive us of his purposes for us on earth nor of our eternal purpose in and through him! How could it? You might say, ‘Oh, of course I follow Christ in these things!’ Well, why do you then quote the thoughts and attitudes of the power of positive thinking (which originate from ungodly men) instead of the word of God?
Of course, people try to validate this kind of apostasy from the word of God by quoting the Bible! So they quote Psalm 37 and verse four where it says, ‘Delight yourself also in the Lord and he will give you the desires of your heart.’ And then they say, ‘You see, God wants to give you the desires of your heart!’ And by believing this they open the door to every personal dream and ambition that they have without a true consideration of what God’s will for their lives is! And they forget the first part of the verse which says, ‘delight yourself in the Lord!’ The problem is, at the heart of the matter, that many believers delight themselves IN THEIR OWN AMBITIONS AND DREAMS! And then use this verse to pursue them! If you delight yourself in the Lord, if he himself is your joy and your love, then it will be natural to you to seek his will and to do his will in your life! As the psalmist said, ‘I delight to do your will, O my God: yea, your law is within my heart.’ (Psalms 40:8). People are turning things upside down today and delighting themselves in something else other than God!
Many young Christians are falling into the trap that the apostle James warns against! In his letter in chapter 4 verses 13 to 16 he says this, ‘ Come now, you that say, Today or tomorrow we will go into such a city, and continue there a year, and buy and sell, and get gain: Whereas you know not what shall be tomorrow. For what is your life? It is even a vapour, that appears for a little time, and then vanishes away. For you ought to say, If the Lord wills , we shall live, and do this, or that. But now you rejoice in your boastings: all such rejoicing is evil .’
You see, even in New Testament times believers got caught up with their ‘dreams’ and ‘ambitions’. They were SO OCCUPIED with making a ‘success’ of their business and careers, that they LEFT GOD OUT of their planning! Even so today, many believers are boasting and rejoicing in the idea that they can fulfil their ambitions and their ‘destinies’ by their positive thinking, by never giving up, by never being discouraged by anything! The word of God says that all such boasting and rejoicing is evil. That’s the plain and simple truth. Let us be clear, very clear, it is not a question about whether you can have plans for the future or not, but whether you take account of God and his will for your life in the things you plan! James wasn’t criticising people for having a plan, he was rebuking them for not taking account of God and his will! He was rebuking them for being captivated by the idea of success and a successful future, and forgetting God in the process! Putting your trust in God doesn’t mean turning off your brain like you turn off computer; it doesn’t mean you stop making decisions or plans; it doesn’t mean becoming lazy; it doesn’t mean you can’t take up opportunities that come along! It means you take account of God and his will in everything you do. It means presenting yourself as a living sacrifice with regard to every major step in your life, seeking his confirmation and approval – or his redirection! It means making sure that the opportunity that presents itself to you is the one that God has provided for you!
This takes away all the slavery to positive thinking! ‘I have to keep positive, I have to keep the right attitude, I mustn’t give up, I mustn’t get discouraged etc etc.’ If your life is committed to him and if you commit each step you make to him and seek his confirmation and direction, then you can have PEACE in your heart, a peace that passes all understanding, you can have the joy and confidence that comes from knowing you are in his will! This peace and confidence is the ASSURANCE AGAINST all discouragement and difficulties that arise! Your ‘victory’ does not issue out your ‘positive thinking’, it stems from YOUR CONFIDENCE IN GOD! You can now be freed from all that hard-working mental activity about ‘being positive’, and replace it with a deep trust and confidence in God, who may lead you in the way you would choose, but who may choose not to lead you that way but in another direction! Are you prepared to live like that or not?
Some people give the impression that if you don’t employ ‘the power of positive thinking’ in your attitude, that it means you become passive, carried along by life circumstances – you don’t know where! To think like that is not to think, is not to use our brains! The Bible is full of exhortations and encouragement!
We are told in Romans 12:11 not to be lazy but to be diligent in the things that we do, and that everything we do whether in word or action, we should do ‘all in the name of the Lord Jesus giving thanks to God and the Father by him.’ (Colossians 3:17). Paul tells the Thessalonians that if anyone is lazy and doesn’t work then this person shouldn’t eat either (2 Thessalonians 3:10). Concerning our future and the will of God for our future the Bible does not tell us ‘to think positively’, it does not tell us to have ‘a positive attitude’ in order to ‘succeed’. Concerning the will of God and our future, what we need is to have our ‘minds renewed’ – that is the teaching of the Bible! So we read in Romans 12:1,2,
‘I beseech you therefore, brethren, by the mercies of God, that you present your bodies a living sacrifice, holy , acceptable unto God, which is your reasonable service. And be not conformed to this world: but be transformed by the renewing of your mind, in order that you may prove what is that good, and acceptable, and perfect, will of God .’
Do you think that your hopes and ambitions and destiny are under threat if you do this? It would seem that many do think this, since they are always quoting from the power of positive thinking! How can you be renewed in your mind to know what God’s will is if you fill your heart and mind with the power of positive thinking? That is a sure way of missing God’s will, certainly in this life, and risking the life to come!
As I have said, it is by committing ourselves to Christ continually that we have an understanding and assurance of his good, acceptable and perfect will! THIS is our CONFIDENCE and PEACE in facing any difficulty that may come; it is this confidence and peace that deals with any discouragement that may come! You don’t fight discouragement by fighting discouragement (with your ‘positive’ thinking) but by putting your trust in God. What people and ‘believers’ are posting on facebook and other forums about positive thinking and how everything depends on your attitude, takes God out of the equation, out of people’s thinking, out of people’s lives!
People quote Scripture in order to try to validate the ideas of unbelievers; so for example, they like to quote Proverbs 23:7, where it says, ‘as he thinks in his heart so is he.’ So those who want to exalt self and ignore God’s word say, ‘You see, your attitude is important. How you think in your heart defines you!’ Of course attitude and thinking is important, vitally important! But it is the word of God that is to shape our attitude and thinking! The word of God directs us to the kind of attitude we should have and the kind of thinking we should be engaged in! We are to have faith in Christ and to trust God in all things! This is a foundational attitude! We are to rejoice in Christ Jesus always! With regard to our thinking read Philippians 4:8 where it says, ‘Finally, brethren, whatsoever things are true, whatsoever things are honest, whatsoever things are just, whatsoever things are pure, whatsoever things are lovely, whatsoever things are of good report; if there be any virtue, and if there be any praise, think on these things.’ I suppose to many this verse doesn’t appeal so much as thinking positively about how successful your career is going to be!
With regard to attitude we have a clear instruction in Philippians chapter 2, where Paul says in verse five, ‘let this mind be in you which was also in Christ Jesus.’ What an amazing verse that is! To have the same attitude as Christ. Is that the attitude you want? Read the first half of this chapter to get the full context and blessing! If you want to change your attitude, what about adopting the attitude of the apostle Paul, who says in Philippians chapter 3, in verses seven and eight, ‘But what things were gain to me those I counted loss for Christ. Yea doubtless, and I count all things but loss for the excellency of the knowledge of Christ Jesus my Lord: for whom I have suffered the loss of all things, and do count them but dung, that I may win Christ.’ Is that your attitude – in comparison to knowing Christ, everything else is just dung?
People talk about achieving their goals. Well, the apostle Paul had a goal. Paul had one goal, one aim. He said, ‘Brethren, I count not myself to have apprehended: but this one thing I do, forgetting those things which are behind, and reaching forth unto those things which are before, I press toward the mark for the prize of the high calling of God in Christ Jesus . (Philippians 3:13-14). So if you believe we need to change our attitude, is this the attitude you believe we need to have? Is this your attitude; is this your goal? Or do you think this attitude is just for apostles? But read the next verse and you will see it’s not just for apostles but Paul wants everyone to have this attitude! Paul says if you want to have the right attitude, if you would be perfect in your thinking, if you want to have the right attitude, then this is the attitude you should have!
What is the will of God for your life? The word of God tells you, ‘For this is the will of God, even your sanctification, that you should abstain from fornication.’ (1 Thessalonians 4:3). If you fall into fornication while pursuing your successful career, how will your successful career save you in that day? What is the will of God for my life? He tells me, ‘Rejoice evermore. Pray without ceasing. In everything give thanks: for this is the will of God in Christ Jesus
concerning you .’ (1Thessalonians 5:16-18). You might ask me, “What has this to do with my future career?” Well, it has EVERYTHING to do with your future! If you don’t have the right relationship with God, if you don’t have the right attitude towards God, if you are not walking in fellowship with God and committing your life continually to him you will MISS his will for your life! Or have you made future success and idol in your life?
Many Christians shamelessly teach things like, “You need to discover your purpose in life; you need to fulfil your destiny in life! If you don’t know your purpose in life how can you fulfil your destiny?” This is nonsense! Christians talk as if there is no Bible and no God! Our destiny on earth and in eternity is made clear from the first chapters of the Bible, where God says, “let us make man in our own image.” God’s eternal purpose for you and me is to be made in his image, to shine in his image! “For whom he did foreknow, he also did PREDESTINATE TO BE CONFORMED TO THE IMAGE OF HIS SON, that he might be the firstborn among many brethren. (Romans 8:29; read also 2 Corinthians 3:18 and 1 John 4:17). We are to be as Christ on earth and in eternity! This is our destiny! How can people TRIVIALISE the great calling of God on our lives and reduce and corrupt its meaning to apply a temporary career or business we might have on earth?
What is the purpose of eternal life? Jesus Christ gives us a clear answer in John 17:3, where he says, “And this is life eternal, that they might know you the only true God, and Jesus Christ, whom you have sent.” Our purpose in time and in eternity is to know the Father and to know the Son! The devil wanted to destroy God’s purpose for Adam and Eve on earth and he enticed them by quoting something that was true (in part!). And the devil wants to do the same in your life by enticing you with the teaching of the power of positive thinking – and it seems he is succeeding in many lives! And there are preachers today that do this very thing, namely, they teach a self-centred gospel about positive thinking and success and make it enticing by quoting and corrupting a few Scriptures to support these deceptions.
God is well able to sort out and direct my life in the path that he has chosen with regard to any job of future activity I might be involved in! This is incidental to the great calling with which he has called you and me in Christ Jesus! If I put my trust in Christ and commit my life and every step I take to him, then he is well able to lead me into the job or career that he wants me to do and to bless me! But my job, career or business is not my life’s purpose nor is it my destiny! Christ is my destiny – in this life and in eternity! To be like him, and manifest his life on earth in everything that I do – that is my purpose and my destiny! Christians are turning to the world’s philosophy and teaching things that rob Christians not only of God’s eternal purpose and destiny for them but also of God’s will for them on earth by filling their heads and hearts with the ideas of the power of positive thinking that focuses on their abilities, their decisions and their attitude rather than focusing on TRUSTING in God, COMMITTING one’s life to him at every step and letting him CONFIRM his will for our lives.
Let me just say, in case someone misunderstands me, that the alternative to having what they call a ‘positive attitude’, is not being negative, feeling useless and hating yourself! Because this too is the devil’s work! The alternative is putting our hope and trust completely in Jesus Christ who loved us and gave himself for us that we might have life, and have it more abundantly! God can make a way for us through the most impossible situations (Isaiah 43:1-3,16). The Scriptures that exhort and encourage us to put our trust in God are too numerous to mention here! If you want your thinking to be ‘positive’ in the biblical sense, then what you need to do is to put all your trust in the living God!
This is what the apostle Paul did and that’s why he could say in Philippians 4:13, ‘I can do all things through Christ who strengthens me.’ But what are the ‘all things’ that Paul mentions here? This is what he says, ‘I know both how to be abased, and I know how to abound: everywhere and in all things I am instructed both to be full and to be hungry, both to abound and to suffer need.’ Paul was prepared for, and content in any situation! He can do these all things through Christ! Many people will not like this because putting your trust in Christ does not always lead to what people consider success or being successful. And here we have the fundamental reason why they turn their back on God’s word and embrace the teaching of the power of positive thinking which in general leaves out references to God and to Christ! They say things like ‘just change your attitude and you will find success; have confidence in yourself and you will succeed!’ In many of their statements they leave out the reference to God and to Christ since there one aim is not Christ but a successful business or career! Or these false preachers will simply corrupt God’s word and so you will find total nonsense posted on Facebook, like for example, ‘God has confidence in you, so have confidence in yourself.’ God has confidence in you? Where do they get this from? Why do believers swallow this poison? God loves us and has given us the most precious thing that he has, namely his son Jesus Christ, because our lives were lost in sin and darkness, so that we might now put our trust completely in him who alone is worthy! That’s why Paul says in Philippians 3:3, “For we are the circumcision, who worship God in the spirit, and rejoice in Christ Jesus, and have no confidence in the flesh.” These are the characteristics of the true Christian! Life’s difficulties are to teach is one thing, namely, “that we should not trust in ourselves, but in God
who raises the dead.” (2 Corinthians 1:9).
Please let me be clear. The question is not whether we use our abilities or not, IT IS A MATTER OF WHERE WE PUT OUR TRUST. You see, the choice is not between confidence or no confidence, but putting our confidence in God!
Coming to God about these matters to find his good, acceptable and perfect will, means that at times we might find that His will is different to what is in our hearts, and if we are to live before him as a living sacrifice, then we should be prepared for this. Many years ago I very much wanted to pursue a particular course of action in my life, a very important one, but as I waited on God it became increasingly clear that it was not the way that God wanted me to go. Often God confirms his will by the peace that he gives us in our hearts, or by the total lack of peace! And I simply had no peace in my heart to take the step, although I thought it was the perfect timing and opportunity! How thankful I am today that I didn’t take that step, which I can now see, looking back, would have been disastrous for me! What a wonderful God we have! What a wonderful father we have, who so cares for us and who can direct us in the important decisions of our lives! He sees and knows things that we can’t possibly know or foresee! But this is only possible if we present our bodies and our lives as a living sacrifice before him and put our trust wholly in him! I trust these few words will encourage you to put your trust in Him. Amen.